Mfululizo wa Mafundisho katika Teolojia Pangilifu SOTERIOLOJIA: MAFUNDISHO YA KIKRISTO KUHUSU WOKOVU [1, 1 ed.] 9789976572636

Na Mwandishi: Huu ni mfululizo wa masomo katika uwanja wa “Teolojia Pangilifu” (Systematic Theology). Sasa tunashughulik

816 182 564KB

Kiswahili Pages 154 Year 2021

Report DMCA / Copyright

DOWNLOAD FILE

Polecaj historie

Mfululizo wa Mafundisho katika Teolojia Pangilifu 
SOTERIOLOJIA: MAFUNDISHO YA KIKRISTO KUHUSU WOKOVU [1, 1 ed.]
 9789976572636

Table of contents :
Yaliyomo
TABARUKU i
UTANGULIZI ii
Yaliyomo vi
SURA YA KWANZA 1
Maana ya soteriolojia 1
Kila Dini Hutafuta Wokovu 4
Hitaji la Wokovu kwa Mwanadamu 7
Mpango wa Wokovu wa Mungu kwa Wokovu wa Mwanadamu 10
Mungu alijua mapema kila kitu 12
Mpango wa Kusudi la Mungu la Milele 19
Wito wa Kupokea Wokovu 21
SURA YA PILI 25
MPANGILIO WA WOKOVU 25
SURA YA TATU 34
KUCHAGULIWA MAPEMA NA KUITWA 34
a. Kuchaguliwa 34
Dhana potofu kuhusu kuchaguliwa mapema 42
Majibu kwa dhana potofu 44
Ni Wateule tu. 46
b. Kuitwa 55
Maswali fikirishi 66
SURA YA NNE 67
KUZALIWA UPYA NA KUHESABIWA HAKI 68
a. Kuzaliwa Upya 68
b. Kuhesabiwa Haki 75
SURA YA TANO 88
TOBA NA UTAKASO 88
a. Toba 88
b. Utakaso 97
SURA YA SITA 103
KUFANYWA WANA 103
SURA YA SABA 111
KUHIFADHIWA, UHAKIKISHO NA KUTUKUZWA 111
a. Kuhifadhiwa 111
b. Uhakikisho 122
c. Kutukuzwa 127
SURA YA NANE 129
TULIP 129
T-Total depravity (Upotovu Kamili) 130
U-Unconditional election (Uchaguzi usiokuwa na masharti) 132
L-Limited atonement (Upatanisho wenye Mipaka) 133
I-Irresistible grace (Neema Isiyoweza Kuzuiliwa) 134
P-Perseverance of the saints (Uvumilivu wa Watakatifu) 135
Marejeleo 138

Citation preview

SOTERIOLOJIA MAFUNDISHO YA KIKRISTO KUHUSU WOKOVU

TEOLOJIA PANGILIFU-2

1

Hakimiliki © 2020 Daniel John Seni Chapa ya January, 2021

Msanifu: Eternal Word and Charity Publishing (EWCP). Dar es Salaam [+255-755-643-590] Mchapaji: Truth Printing Press. Dar es Salaam [+255764425704] ___________________________________ Haki zote zimehifadhiwa. Hakuna sehemu ya chapisho hili inayoweza kuzalishwa tena, au kuboreshwa au kusambazwa kwa njia yoyote au kwa kubadilisha umbo au kunakili na kupeleka katika umbo lingine bila idhini ya mwandishi. _______________________________________ Maandiko ya Biblia yamechukuliwa kutoka kwenye Biblia ya Kiswahili Toleo la shule inayotolewa na Swahili Union Version (SUV). Tafsiri iliyotumika kwenye marejeleo yaliyokuwa kwenye lugha ya kiingereza si tafsiri rasmi; hivyo inaweza kuendelea kuboreshwa kwa kila chapa ya kitabu hiki. ________________________ Msambazaji Shekinah Mission Centre (SMC) [email protected] S.L.P 32807 Dar es Salaam +255 769 080 629 +255 787 907 347 Madale/Mivumoni, Joshua road, mkabala na Shule ya Msingi-Atlas/ at Shekinah Presbyterian Church in Tanzania, Dar es Salaam

TABARUKU Kwa wanazuoni wote wa teolojia

i

UTANGULIZI Huu ni mfululizo wa masomo katika uwanja wa

“Teolojia

Pangilifu”

(Systematic

Theology). Sasa tunashughulikia somo la Soteriolojia, yaani somo linalohusu “wokovu wa mwanadamu.” Siku

hizi

pengine

inaweza

kudhaniwa

kwamba kila Mkristo anajua maana ya wokovu na upatikanaji wake. Watumishi wengi wasiopenda kujishughulisha huishia kusema “Yesu anaokoa” bila kufafanua maana ya sentensi hii nyepesi na rahisi sana.

Ni

misiolojia

kweli

katika

tunaweza

muktadha

kutumia

wa

sentensi

nyepesi kama hizi bila kuzitolea ufafanuzi kwa

sababu

tunachukulia

wale kwamba

chochote.

ii

tunaowaambia hawajui

kitu

Siku

hizi

“makanisa

kuna ya

makanisa

wokovu”

yanayojiita,

ambayo

hudai

kuhubiri wokovu wa kweli. Hata hivyo, nimegundua mafundisho

mapungufu yao

mengi

kuhusu

katika

wokovu

kwa

kudhania kwamba wokovu ni tukio la sekunde moja. Ama kwa hakika, wokovu ni mchakato; ingawa

yawezekana

michakato

hiyo

isipangiliwe vizuri na kuleta maana, lakini bado tunapaswa kujua kwamba wokovu ni mchakato. mwanadamu

Mchakato

wa

unaanzishwa

kumwokoa na

Mungu

mwenyewe na kumaliziwa pia na Mungu mwenyewe. Katika kitabu hiki, kwa namna ya upekee nimejaribu kufafanua kwa undani kuhusu michakato hiyo kwa kuzingatia ufafanuzi

iii

wa

teolojia

iliyoboreshwa

(Reformed

Theology) Kitabu

hiki

wameshazaja

si

kwa

akili

wale

zao

ambao

mafundisho

mbalimbali ya wokovu, na hivyo hawataki kubadilisha mwelekeo na kujifunza upya. Pia kitabu hiki si kwa wazembe, wasiopenda kushughulisha

akili

zao.

Si

kwa

wale

wanaopenda kutafuniwa tu, bali ni kwa wale ambao wanaweza kuvunja mifupa na kuelewa. Ninakutia moyo kwamba unaposoma kitabu hiki

unahitaji

kusoma

katika

hali

ya

utulivu, na kumwomba Roho Mtakatifu akusaidie ili uweze kuelewa zaidi na zaidi somo hili muhimu. Marejeleo mengi yaliyotumika katika kitabu hiki yanatokana na lugha ya Kiingereza, iv

hivyo basi, kwa wale ambao wana uwezo wa kusoma Lugha ya Kiingereza wanashauriwa kupata baadhi ya nakala za vitabu hivyo kwa sababu ni muhimu sana. Yawezekana katika kitabu hiki ninaweza nisikubaliane na baadhi ya tafsiri ya kambi ya Teolojia Iliyoboreshwa kwa asilimia zote, lakini

kwa

kweli

kwa

sehemu

kubwa

inakubaliana na mafundisho halisi ya Neno la Mungu.

v

Yaliyomo TABARUKU .................................................i UTANGULIZI .............................................. ii Yaliyomo ................................................... vi SURA YA KWANZA .....................................1 Maana ya soteriolojia ...............................1 Kila Dini Hutafuta Wokovu ......................4 Hitaji la Wokovu kwa Mwanadamu ..........7 Mpango wa Wokovu wa Mungu kwa Wokovu wa Mwanadamu .......................10 Mungu alijua mapema kila kitu .............12 Mpango wa Kusudi la Mungu la Milele ..19 Wito wa Kupokea Wokovu......................21 SURA YA PILI ...........................................25 MPANGILIO WA WOKOVU ........................25 SURA YA TATU .........................................34 KUCHAGULIWA MAPEMA NA KUITWA .....34 vi

a.

Kuchaguliwa ..................................34

Dhana potofu kuhusu kuchaguliwa mapema ................................................42 Majibu kwa dhana potofu ......................44 Ni Wateule tu.........................................46 b.

Kuitwa............................................55

Maswali fikirishi ....................................66 SURA YA NNE ..........................................67 KUZALIWA UPYA NA KUHESABIWA HAKI 68 a.

Kuzaliwa Upya................................68

b.

Kuhesabiwa Haki ...........................75

SURA YA TANO ........................................88 TOBA NA UTAKASO .................................88 a.

Toba ...............................................88

b.

Utakaso ..........................................97

SURA YA SITA ........................................ 103 vii

KUFANYWA WANA ................................. 103 SURA YA SABA ...................................... 111 KUHIFADHIWA, UHAKIKISHO NA KUTUKUZWA ......................................... 111 a.

Kuhifadhiwa ................................. 111

b.

Uhakikisho ................................... 122

c.

Kutukuzwa ................................... 127

SURA YA NANE ...................................... 129 TULIP ..................................................... 129 T-Total depravity (Upotovu Kamili) ....... 130 U-Unconditional election (Uchaguzi usiokuwa na masharti) ........................ 132 L-Limited atonement (Upatanisho wenye Mipaka) ............................................... 133 I-Irresistible grace (Neema Isiyoweza Kuzuiliwa) ........................................... 134

viii

P-Perseverance of the saints (Uvumilivu wa Watakatifu) .................................... 135 Marejeleo ................................................ 138

ix

SURA YA KWANZA DHANA YA WOKOVU Maana ya soteriolojia Soteriolojia (Kiingereza Soteriology) ni tawi la teolojia linahusika na wokovu. Neno hili

linatokana

na

neno

la

Kigiriki

“soterion” lenye maana ya "wokovu," na pia linahusiana na neno “soter,” yaani "mwokozi."1

Mtu

mwingine

huenda

akajiuliza, ya nini kuandika maneno ya Kigriki katika andiko la Kiswahili? Ni sahihi kujiuliza hivyo, lakini ikumbukwe kwamba Biblia katika Agano Jipya iliandikwa kwa Kigiriki kabla ya kutafsiriwa katika lugha za makabila mbalimbali duniani, kwa sababu hiyo kurejelea maana ya neno kwa asili yake inasaidia

kuelewa

vizuri

Bruce Demarest, The Cross and Salvation (Wheaton: Crossway Books, 1997), 28-29 1

1

kile

kilichokusudiwa awali. Hata hivyo maneno haya mara nyingi yanakuwa ni ya kitaaluma sana; hivyo basi ili kusaidia watu wote waweze kuelewa, na kwa kuwa “soteriolojia” ni neno la kitaaluma, basi katika kitabu hiki tutatumia neno ambalo ni mbadala wake kwa Kiswahili, yaani “Wokovu.” Soteriolojia ni somo linaloshughulikia uwasilisho

wa

baraka

za

wokovu

kwa

mwenye dhambi na kurudishiwa upendeleo wa kimungu katika ushirika wa karibu na Mungu. Huonyesha ujuzi wa Mungu kama chanzo cha kutosha cha maisha, nguvu na furaha ya wanadamu. Inafaa zaidi kujifunza “soteriolojia”

ukiwa

umekamilisha

kujifunza “Kristolojia” Wanazuoni wengi huweka “soteriolojia” pamoja na “pneumatolojia” (Elimu kuhusu Roho Mtakatifu) kwa sababu inaaminika 2

kwamba “soteriolojia” ni kazi ya Roho Mtakatifu kutumia kile ambacho Kristo amekinunua pale msalabani kwa ajili ya Wateule wake. Roho Mtakatifu anaweka wokovu kwa Wateule kwa wakati ambao umeamriwa na Mungu Baba. Kitu ambacho hapa

ninaweza

kusema

ni

kwamba

“wokovu” ni tendo zima la Utatu wa Mungu. Kwamba Mungu Baba anachagua wateule, Yesu Kristo ananunua wokovu wao, na kisha Roho Mtakatifu anautumia wokovu huo kwa Waamini. Wokovu ni tukio na mchakato

ambao

watu

huletwa

katika

uhusiano mzuri na Mungu. Mafundisho kuhusu wokovu yanaweza kuonekana kama rahisi na mepesi sana, lakini yamekuwa na changamoto kubwa katika Ukristo. Si katika Ukristo peke yake, katika dini mbalimbali duniani wokovu wa 3

mwanadamu ni ajenda ambayo haielezeki kirahisi. Somo hili ni nyeti sana kiasi kwamba linashikilia mandisho mengine ya Biblia.2 Kila Dini Hutafuta Wokovu Dhambi imetafuna sehemu zote za mwanadamu,

na

matokeo

yake

kila

mwanadamu kwa namna fulani hujaribu kutafuta wokovu kwa njia ambayo anaona yeye ni sahihi. Kwa hiyo kiini cha kila dini ni kutafuta wokovu. Dini zote hutafuta njia ya wokovu; wanadamu wote wanatamani furaha kwa sababu moyo wa mwanadamu umeumbwa kwa ajili ya Mungu na hauwezi kupumzika mpaka

amupate

(Augustine).

Walakini,

katika giza la ufahamu wetu na mawazo Samuel Waje Kunhiyop, African Christian Theology (Kenya: HippoBooks, 2012) 77. 2

4

mabaya ya mioyo yetu, hatumtafuti kwa njia sahihi. Dini za kipagani hazina dhana juu ya utakatifu wa Mungu; hawaelewi dhambi sawasawa na hawajui chochote kuhusu

neema.

Hawamjui

Kristo,

wanatafuta wokovu kwa njia ya matendo. Buddha mwanafunzi

aliwahi wake,

kumwambia

“Kuwa

nuru

mwenyewe!"

“Kuwa

kimbilio

mwenyewe.

Usikimbilie

kitu

chochote.

Shikilia

ukweli

yako lako

kingine

kama

taa.

Usitafute kimbilio kwa mtu mwingine yeyote isipokuwa wewe mwenyewe.”3 Kwa hiyo kwa mujibu wa dini ya Buddhism kila mtu ni mwokozi wake mwenyewe. Hakuna mtu au mungu

anayeweza

kumwokoa

mtu

mwingine zaidi ya mtu mwenyewe.

Bavinck, Herman. Reformed Dogmatics (pp. 473-474). Baker Publishing Group. Kindle Edition. 3

5

Katika

Uislam,

mtu

anakombolewa

kwa kumwamini Mungu mmoja na mtume Muhammad

kama

nabii

wake

na

kwa

kufanya majukumu ya kidini kama vile sala, sadaka, kufunga, kuhiji. Kwa hiyo kwa mujibu wa Waislam wokovu si zawadi, bali ni matendo binafsi ya mtu, ni juhudi zako binafsi ambazo zinakufanya uepuke adhabu ya kuzimu. Dini

nyingi

zinatafuta

ukombozi

kupitia hatua za wanadamu. Kwa maana hiyo,

dini

hizi

zinawataka

wanadamu

kutimiza sheria fulani iliyowekwa. Mkazo wa maadili

na

matendo

ndiyo

husisitizwa

katika dini hizi kwa ajili ya kuwapatia watu wokovu wao wa milele. Kwa hakika maisha ya baadaye huangaliwa kwa umakini na hivyo mtu kuishi maisha ya mzigo kwa ajili ya kujaribu kupata wokovu kwa njia yake 6

binafsi.

Mara

nyingi

utasikia

watu

wakisema, “wokovu ni matendo tu.” Au “wokovu ni wewe mwenyewe tu ulivyojiweka kwa

Mungu.”

Au

utasikia

wapendwa

wakisema “shikilia wokovu wako.” Katika mawazo

haya

mwanadamu

wokovu sana,

unaegemea

badala

ya

kwa

Mungu.

Mungu ni hakimu tu, wa kuangalia makosa ya mwanadamu na kuhukumu; rehema na neema zake zinaachwa. Mpango wake wa wokovu kwa wanadamu haujulikani katika dini nyingi kwa sababu shetani ameelekeza moyo wa wanadamu huko. Utafutaji wa wokovu kwa njia za wanadamu katika dini nyingi huonesha wazi kwamba mwanadamu anahitaji wokovu. Hitaji la Wokovu kwa Mwanadamu Wokovu si tukio la kushtukiza kwa Mungu,

bali

Mungu 7

kwa

kusudi

lake

takatifu, aliruhusu mwanadamu aanguke katika majaribu katika Bustani ya Edeni, na hivyo dhambi iliingia ulimwenguni. Dhambi ilisababisha utengano kati ya Mungu na mwanadamu, na hivyo, “…wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.” (Rum 3:23). Nabii Isaya 59:2 anatuambia

“Lakini

maovu

yenu

yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi

zenu

zimeuficha

uso

Wake

msiuone, hata hataki kusikia.” Kwa nukuu hizi, hakuna mwanadamu ambaye anaweza kujiokoa

mwenyewe.

Hakuna

ambaye

anaweza kutimiza matakwa ya sheria ya Mungu. Kuna mawazo mbadala kwamba hitaji la wokovu si kwa mwanadamu peke yake, hata kwa viumbe wengine nao wanahitaji wokovu.

Wanaosisitiza 8

hili

wananukuu

Warumi 8:19-22 “Kwa maana viumbe vyote pia

vinatazamia

kwa

shauku

nyingi

kufunuliwa kwa wana wa Mungu. Kwa maana viumbe vyote pia vilitiishwa chini ya ubatili; si kwa hiari yake, ila kwa sababu yake yeye atiyevitiisha katika tumaini; kwa kuwa viumbe vyenyewe navyo vitawekwa huru

na

kutolewa

katika

utumwa

wa

uharibifu, hata viingie katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu. Kwa maana twajua ya kuwa viumbe vyote pia vinaugua pamoja, navyo vina utungu pamoja hata sasa.” Japokuwa kuashiria

fungu

uumbaji

kurejeshwa

upya,

hilo

linaweza

mwingine

kuhitaji

haimaanishi

kwamba

vinahitaji wokovu kama ulivyo wokovu wa wanadamu; bali vitafurahia matunda ya wokovu

wa

mwanadamu 9

wakati

wa

kutukuzwa. Kwa hiyo katika maisha haya viumbe vingine havihitaji wokovu kama ilivyo kwa mwanadamu. Mpango

wa

Wokovu

wa

Mungu

kwa

Wokovu wa Mwanadamu Mara

nyingi

maneno

"mpango

wa

milele wa Mungu wa wokovu" hutumiwa katika uinjilishaji kwenye zile karatasi kwa kutaja vitu vitatu au vinne Mungu anataka mtenda dhambi afanye ili aweze kuokolewa, kwanza, Tambua kwamba wewe ni mwenye dhambi na unahitaji wokovu, pili, amini kwamba Yesu alikufa msalabani kwa ajili ya dhambi

zako,

tatu,

Muombe

Mungu

akusamehe dhambi zako, nne, mtumaini Yesu.

na

baada

ya

hapo

mhusika

anasalishwa sala ya toba. Mambo haya ni ya muhimu, lakini hayaonyeshi mpango wa Mungu wa wokovu. Ni taratibu nzuri katika 10

kuelewesha mtu aitikie mwito wake, lakini huenda isieleze usahihi wa mpango wa Mungu wa wokovu. Neno wokovu laweza kuonekana kuwa ni rahisi lakini kwa kweli linajumuisha dhana nyingi ambazo haziwezi kueleweka kikamilifu kwa akili ya kawaida. Tunaweza kujiuliza maswali ya kawaida tu, Je, wokovu ni kwa ajili tu ya kuikimbia jehanamu? Je, ni jambo ambalo Mungu alihitaji kulifikiria wakati Adamu na Hawa walipomwasi? Je Mungu

kweli

wataokoka

anajua

kwa muda

ni

akina

nani

gani? Jambo

la

kuzingatia katika maswali haya ni kuwa Biblia

inatufundisha

kwamba

Mungu

alipanga wokovu wetu kabla ya msingi wa ulimwengu, kwa kuwa anajua mambo yote, alijua kwamba mwanadamu atauhitaji, na

11

huu si utabiri wa Kimungu, bali ni ujuzi wa mapenzi yake yasiyo na kipimo. Mungu alijua mapema kila kitu Katika WCF/3/14 Tunasoma, “tangu asili, Mungu ameamua na kuweka kila kitu kinachotokea. Yeye hufanya maamuzi haya kwa uhuru kwa mapenzi Yake ya busara na utakatifu. Hakuna kitu ambacho ameamua tangu asili kinaweza kubadilika. Maamuzi haya haimaanishi kwamba Mungu ndiye mwanzilishi wa dhambi na kwamba Yeye hatulazimishi kufanya vitu kinyume cha mapenzi yetu. Yeye ndiye chanzo cha kila kitu, lakini hii haimaanishi kwamba vitu vingine havijahusika; hata hivyo, Mungu ndiye sababu ya vitu vingine kuwepo.” Kitabu hiki katika lugha kimetafsiriwa kama “Misingi ya Imani: Mafundisho ya Msingi ya Kibiblia: Kuhusu Imani Ya Kikristo.” The Westminster Confession of Faith and Large Catechism. Kimefasiriwa na D.J. Seni, 2020. Katika kifupisho hicho WCF/sura/sehemu 4

12

Hoja hii iko katika “amri za Mungu”5 (kiingereza “God’s decrees”) maana yake ni kusudi lake au uamuzi wake kwa mambo yajayo; au, shauri la uamuzi wake, ambalo tangu milele aliamua mapema chochote atakachofanya, au anachoruhusu kufanywa au kufanyika kwa wakati. Ufafanuzi huu huenda sambamba na ukweli linaweza

kwamba

hakuna

kumshangaza

jambo Mungu

ambalo pale

linapotendeka kana kwamba ni jipya na kwamba alikuwa hajui kama litatendeka. Tujue kwamba, “hakuna dhambi, ambaye inaweza kufanyika, hata ile ambayo tayari imeshafanyika Mungu hakujua.”6 Kwa hiyo Neno “amri za Mungu” hapa si zile amri kumi. Mara nyingi linapokuja suala la amri kumi huwa zinaandikwa kwa pamoja kwa kirai, “amri kumi” na kama hakuna neno la amri kumi basi pengine yaweza kuwa ni decree au laws nk. 6 Brown, John. Systematic Theology: A compendious View of Natural and Revealed Religion (Grand Rapids: Reformation Heritage Books, 2002) uk. 159. 5

13

amri ya Mungu inahusu mambo yajayo ambayo Mungu anayajua tangu asili. Pamoja na kuwa Mungu alipanga kila kitu, na kwamba yeye ni sababu ya kila kitu; haimaanishi kwamba “sababu ya pili” (second cause) haipo. Kwa mfano ingawa Mungu alijua kwamba kuna anguko, si kwamba aliwatega Adamu na Hawa ili waanguke, bali kwa uhuru wao wenyewe, waliruhusu majaribu ya Shetani (sababu ya pili kwenye anguko); basi wakaanguka. Na kwa sababu hiyo Mungu halaumiwi kwa anguko lakini bado anajitukuza katika hilo. Kwa hiyo uweza wa Mungu na mapenzi yake

vinafanya

ajue,

na

kung’amua

mapema kuhusu wokovu wa mwanadamu. Hata hivyo, kama tulivyoeleza hapo juu, visababishi

vya

pili

(second

cause)

vinasababisha. Hata visababishi vya pili, 14

bado vimo katika mpango wake. Mungu anapokuwa ametumia visababishi vya pili haimaanishi kwamba anategemea kiumbe chake chochote au wakala yeyote.7 Ingawa Mungu

anajua

chochote

kinachoweza

kutokea katika hali zote zinazowezekana hata hivyo, hajaamuru chochote kitokee kwa sababu aliona tangu asili kwamba kitatokea kwa namna yoyote ile. Mwanadamu

baada

ya

anguko

alipotoka kabisa, “hali nzima imeharibiwa na dhambi, na dhambi hiyo imeenea kwa watu wote na katika maeneo yote kiasi kwamba hakuna kitu kwa mwanadamu

Brown, John. Systematic Theology: A compendious View of Natural and Revealed Religion (Grand Rapids: Reformation Heritage Books, 2002) uk. 149. 7

15

ambacho

kinaweza

kumfanya

akubalike

mbele za macho ya Mungu.”8 Mpango wa wokovu wa mwanadamu ni wa kushangaza, Charles Hodge9 anaweka bayana mchanganuo wa Augustino kuhusu mpango wa Mungu wa wokovu, na hapa chini tutafupisha. 1. Kwamba

utukufu

wa

Mungu,

au

udhihirisho wa ukamilifu wake, ndio Fatima ya juu kabisa na ya mwisho ya vitu vyote. 2. Kwa

hatima

uumbaji

wa

hiyo

Mungu

ulimwengu

alikusudia

na

mpango

mzima wa wokovu. 3. Kwamba Mungu alimweka mwanadamu katika

hali

ya

majaribio,

akimfanya

Charles Ryrie, Basic Theology: A Popular Systematic Guide to Understanding Biblical Truth Kindle Edition 9 Hodge, Charles, Systematic Theology – (Vol. III) (Grand Rapids, MI: Christian Classics Ethereal Library,) 8

16

Adamu, mzazi wao wa kwanza, mkuu wao na mwakilishi. 4. Kwamba anguko la Adamu lilileta wazao wake wote katika hali ya hukumu, dhambi, na taabu, ambapo hawawezi kujikomboa wenyewe 5. Kutoka

miongoni

walioanguka

Mungu

mwa

wengi

alichagua

idadi

isiyohesabika ya watu kwa uzima wa milele, na wengine akawaacha ili wapate malipo ya haki ya dhambi zao. 6. Kwamba msingi wa uchaguzi huu sio utabiri

bali

mwenyewe

ni bila

uamuzi

wa

kuingiliwa

Mungu na

kitu

chochote 7. Kwa wokovu wa wale waliochaguliwa kwa uzima wa milele, Mungu alimtoa Mwanawe

mwenyewe,

kuwa

mwanadamu, na kutii na kuteseka kwa 17

ajili ya watu wake, na hivyo kuleta haki kwao milele na kutoa wokovu wa mwisho kwa wateule. 8. Roho Mtakatifu katika kazi zake za kawaida, yuko kwa kila mtu, maadamu anaishi, na anazuia uovu kuendelea, lakini nguvu zake zenye ufanisi na za kuokoa hutumika kwa wateule. 9. Kwamba

wale

amewachagua, alijitoa

wote kwa

ajili

mwenyewe

ukombozi, wakiwa

hakika

ambao

Mungu

yao

katika

Kristo

agano

(isipokuwa

wachanga),wataletwa

la

wakifa kwenye

ujuzi wa ukweli, kwa mazoezi ya imani, na

kwa

uvumilivu

katika

maisha

matakatifu hadi mwisho. Kwa hakika, huenda Augustino alieleza kwa usahihi kuhusu mpango wa wokovu wa

mwananadamu. 18

Katika

vipengele

vifuatavyo

tutajaribu

kuelezea

kwa

undani mpango huu wa milele ambao Mungu aliuweka tayari kwa ajili ya watu wake. Mpango wa Kusudi la Mungu la Milele Wokovu wa mwanadamu haukuanzia pale

mwanadamu

alipoumbwa,

bali

ni

mpango wa Mungu wa milele, wa tangu asili.

Kwa

mwanadamu

hiyo si

Mungu kwa

anamwokoa

kumwepusha

na

Jehanamu, (ingawa, wasiiokoka wataishia Jehanamu), bali ni “kwa kadiri ya kusudi la milele alilolikusudia Bwana

wetu.”

katika

(Efe.

3:11),

Kristo “kabla

Yesu ya

kuwekwa misingi ya ulimwengu” (Efe. 1:14) Katika Warumi 8:28 Paulo anasema kwamba Wakristo waliitwa "kwa wokovu" kulingana na kusudi lake.” Katika Waefeso 1:11

anasema

kwamba 19

Wakristo

“Walifanywa warithi [wa Mungu], wakiwa wamechaguliwa tangu zamani kulingana na kusudi

lake

yeye

afanyaye

vitu

vyote

kulingana na kusudi la mapenzi yake.” Na katika 2 Timotheo 1: 9 Paulo anathibitisha kwamba “Mungu alituokoa na kutuita sisi kwa

wito

mtakatifu,

sio

kulingana

na

matendo yetu bali kulingana na makusudi yake na neema tuliyopewa katika Kristo Yesu tangu milele. Katika Luka 22:22 Yesu aliwafundisha wanafunzi Mwana

wake

wa

kwamba

Adamu

ilivyokusudiwa

(kama

Mungu).

Petro

kwamba

ingawa

"

aenda

Kwa

kuwa

zake

kama

ilivyokusudiwa

anafafanua Herode,

kwa

Wafalme,

na wazi na

wengineo walihusika katika kifo cha Yesu, walihusika kwa sababu ya kutimiza kusudi la milele la Mungu. Anasema, “ili wafanye 20

yote ambayo mkono wako na mashauri yako yamekusudia tangu zamani yatokee.” (Mdo 4:28) Wito wa Kupokea Wokovu Kwa kweli ningeweza kuita, wito wa kudhihirisha wokovu, lakini kwa sababu za kiteolojia tutumie neno “wito wa kupokea wokovu.” Ingawa Mungu aliandaa kila kitu kwa ajili ya wokovu wa wateule, ni kwa wakati

maalumu

alimua

kufanya

udhihirisho wa kile alichokipanga mapema. Katika WCF/8/1 tunasoma kwamba, “Mungu, katika kusudi lake la milele ilimpendeza Bwana

kumchagua

Yesu,

mpatanishi

Mwana kati

ya

na

kumteua

pekee, Mungu

kuwa na

Mwanadamu…” Mwana wa Mungu, nafsi ya pili ya Utatu, ni Mungu wa milele, ni sawa 21

na

Baba.

Katika

utimilifu

wa

wakati

alichukua asili ya mwanadamu (Gal. 4:4) alichukua sifa muhimu na udhaifu wa kawaida

wa

mwanadamu-isipokuwa

kwamba alikuwa hana dhambi, (Ebr 2:14, 16-17, 4:15) kwa sababu angekuwa na dhambi

asingeweza

kuwa

Mwokozi

wa

wateule. Mwenye dhambi hawezi kumwokoa mwenye

dhambi

asemavyo

mwenzake.

Athanasi,

Kama

akinunuliwa

na

Geoffrey W Bromiley kwamba, “kwa upande mwingine, hakuna mtu anayeweza kufa kwa ajili ya wote na asiharibike.”10 Tunasoma kwamba, Yesu alichukuliwa mimba

kwa

nguvu

ya

Roho

Mtakatifu

tumboni mwa Bikira Mariamu, ambapo alichukua

mwili.

Ingawa

ni

maneno

Geoffrey. W Bromiley, Historical Theological: An Introduction (T&T Clark: Edinburgh,1979) uk. 72 10

22

yaliyozoeleka sana katika Imani ya Mitume, lakini hapa yana maana sana. Maana yake ni kwamba Yesu alizaliwa kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Kwa hiyo, akachukua mwili wa mwanadamu, huku yeye akiwa na asili ya uungu; kwa hiyo Yesu ana asili mbili tofauti - ya Kimungu na ya Kibinadamu. Katika WCF/8/3 tunasoma kwamba, “Yesu

alipofanyika

mwanadamu,

alitakaswa na kutiwa Mafuta na Roho Mtakatifu zaidi ya kipimo. Katika yeye mna hazina zote za hekima na maarifa, na ndani yake ilimpendeza Baba kwamba utimilifu wote ukae.

Kusudi la Mungu lilikuwa

kwamba Yesu, Mtakatifu, asiye na ila, wala uchafu

wowote,

na

amejaa

neema

na

ukweli, atekeleze jukumu lake la kuwa Mpatanishi na Mdhamini. Yesu hakujifanya mwenyewe kuwa Mpatanishi, bali aliitwa na 23

Baba yake ambaye alimpa nguvu zote na uwezo kamili wa kuhukumu.” Kwa hiyo kazi ambayo Yesu alikuja kufanya duniani si kwamba

alishuka

tu;

kama

wengine

wanavyodhani kwamba Mungu aliposhuka duniani alifanyika kuwa Yesu. Yesu Kristo alijitoa kama dhabihu kwa Mungu mara moja na milele kupitia yule Roho wa milele, alitimiza haki ya Baba yake (Rum 3:25-26). Kwa dhabihu yake, alilipa deni letu, lakini pia alitununulia urithi katika

ufalme

wa

mbinguni

ambao

utadumu milele. Kwa kweli, ilikuwa tu baada ya Yesu Kristo kufanyika mwanadamu ndipo kweli tumeokolewa, na tunaweza kusema "malipo yamekamilika". Lakini hata kabla ya hapo, tangu mwanzo wa ulimwengu, watu wa Mungu wameweza kuona wema na nguvu 24

ya kuokolewa. Hii ni kwa sababu Mungu alifunua wokovu wake kwa watu wake kama ambavyo

tunaambiwa

"Mwanakondoo

aliyechinjwa" tangu mwanzo wa ulimwengu. Kwamba Yeye ni Yeye yule jana, leo, na hata milele. Hata hivyo wokovu kamili tunaupata Kupitia Kristo peke yake, aliyefanyika mwili, ukamilifu wa Mungu duniani.

SURA YA PILI MPANGILIO WA WOKOVU Wokovu tofautitofauti;

hutazamwa katika

kwa

nyakati

wakati

uliopo

mkamilifu inaaminika kwamba wokovu ni tukio

moja mwanzoni mwa maisha ya

Kikristo. Katika wakati uliopo unaoendelea inaaminika kuwa ni mchakato unaoendelea katika maisha yote ya Kikristo. Na katika 25

wakati ujao, wanaona wokovu ni tukio la baadaye.

Erickson

anatupa

kwamba,

“Wakristo

wanasema,

"Sisi

ufafanuzi

wengine

tumeokoka.”

huwa Wengine

wanaona wokovu ukiwa katika mchakato "tunaokolewa." Bado wengine wanafikiria wokovu kama kitu ambacho kitapokelewa baadaye - "tutaokolewa."11 Kwa namna fulani kila kundi liko sawa, cha msingi inategemea

mtu

amesimama

kwenye

upande gani anapotoa tafsiri hiyo. Hata hivyo,

tumeshang’amua

tangu

awali

kwamba wokovu ni kazi ya Mungu, siyo ya mwanadamu, na ugawaji wa nyakati kama huo wakati mwingine unaweza kutusaidia tu katika maisha haya na namna ya kuishi ndani ya wokovu, lakini ukweli, Kristo alikamilisha

kazi

yake

ya

wokovu.

Erickson J. Millard, Christian Theology (3rd Ed) (Grand Rapids: Baker Academic, 2013), 826. 11

26

Je

unafikiri sentensi gani ni sahihi katika nyakati tatu katika uzoefu wako binafsi wa wokovu? Kwa kweli, ukiachilia kwamba wokovu wa mwanadamu ni mpango wa Mungu, mpango

huo

unachukuliwa

kama

mchakato; mchakato huu ama unafanyika mara moja, ama kwa utaratibu maalumu. Mpangilio huu kwa kiratini huitwa “ordo salutis”

au

kwa

kiingereza

“order

of

salvation.” Michakato ya Wokovu Sasa tutazingatia kwa njia gani na kwa utaratibu

gani

faida

za

ukombozi

zinatumika kwa wateule. Cheung anasema kwamba, “baadhi ya faida hizi huanza pale mteule

anapomwamini

Kristo.”12

Kwa

Vincent Cheung, Systematic Theology (Michigan: Zondervan Publishing House, 2003), uk. 265 12

27

maneno

mengine

ni

kwamba

hatuwezi

kujua hakika baadhi ya michakato inaanza kufanyika

lini,

wakati

gani.

Kweli

tumeshajua kwamba Mungu alituchagua tangu asili, lakini hatujui udhihirisho wa uchaguzi huo unaonekana wazi lini. Katika sehemu inayofuata, tutaangalia michakato hii kwa ukaribu zaidi. Muhtasari wazi wa matumizi (application) ya ukombozi ni ule wa Warumi 8:29-30, ingawa lazima pia tutakuwa tunaangalia vifungu kadhaa vya kibiblia ili kupata orodha kamili. Warumi

8:29-30

inasema,

“maana

wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi. Na wale

aliowachagua

akawaita;

na

tangu

wale 28

asili,

hao

aliowaita,

hao

akawahesabia aliowahesabia

haki; haki,

hao

na

wale

akawatukuza.

Katika fungu hili kuna michakato minne; kuchaguliwa, kuitwa, kuhesabiwa haki na kutukuzwa. kirefomati

Hata

hivyo

wanaongeza

wanazuoni michakato

wa kwa

utaratibu ufuatao:13 Hata hivyo, wanazuoni hao

pia

wanatofautiana

kidogo

katika

upangiliaji wa michakato hii. Tazama mfano katika chati ifuatayo na ubainishe tofauti zake. MCHAKATO REYMOND, L. ROBERT Kuchaguliwa Mapema Kuitwa Kuzaliwa Upya

Reymond, L. Robert, A New Systematic Theology of The Christian Faith (Nashville: Thomas Nelson Publishers 1998), 720-765 13

29

Kuongoka/Kuokoka Kuhesabiwa Haki Kutakaswa Kuhifadhiwa Kutukuzwa MACARTHUR J na MAYHUE Kuchaguliwa Mapema Wito wenye ufanisi Kuongoka/kuokoka Kuhesabiwa haki Kufanywa wana Kutakaswa Uvumilivu wa watakatifu Kutukuzwa

FRAME M. JOHN14

John M. Frame, Salvation Belongs to the Lord: An Introduction to Systematic Theology (New Jersey: P & R Publishing, 2006), 123. 14

30

Kuchaguliwa Kuitwa Kuzaliwa mara upya Kuhesabiwa haki Utakaso Uhakikisho Uvumilivu wa Watakatifu Kutukuzwa

Ukichunguza utagundua

kwa

umakini

kwamba

jedwali

wanazuoni

hilo hawa

hawatofautiani sana. Vipengele ambavyo wanakubaliana

ni;

1)

Kuchaguliwa

2)

Kuitwa 3) Kuhesabiwa Haki 4) Utakaso 5) na Kutukuzwa. Pengine tuchukulie kwamba Reymond,

L.

Robert

anatumia

neno

“kuhifadhiwa” badala ya “Uvumilivu wa Watakatifu.”

Mkanganyiko

upo

katika

“kuzaliwa upya, kuongoka (kuokoka kama 31

ilivyozoeleka), kuhifadhiwa, Uhakikisho, na kufanywa michakato

wana. yote

Nitajaribu

kuifafanua

ambayo

wanazuoni

wamejadili, ingawa mingine nitajadili kwa ufupi sana. Wana Refomati wengi hutumia WCF kama msingi wa kujadili hoja hizi, Ninakushauri upate kitabu hicho. Pamoja na uchambuzi huo, kuna wengine ambao wanaweka mpangilio wa wokovu mpaka hatua kumi. Kwa mfano Wayne Grudem, yeye anapanga hatua kumi kama ifuatavyo:l. Uchaguzi wa Mungu (chaguo la Mungu la watu kuokolewa) 2. Wito wa injili (kutangazwa kwa ujumbe wa injili) 3. kuzaliwa upya (kuzaliwa mara ya pili) 4. Uongofu (imani na toba) 5. Kuhesabiwa haki (haki ya kisheria) 32

6. Kufanywa wana (ushiriki katika familia ya Mungu) 7. Utakaso (mwenendo sahihi wa maisha) 8. Uvumilivu (kubaki Mkristo) 9. Kifo (kwenda kuwa na Bwana) 10. Kutukuzwa (kupokea mwili wa ufufuo) Kwa hakika, huenda mpangilio wa Grudem unapendwa na wanausasa kwa sababu kuna

hatua

ambazo

zimeongezwa.

Mwenyewe anafafanua kwamba “Tunapaswa kutambua hapa kwamba namba 2 hadi 6 na sehemu ya 7 zote zinahusika katika "kuwa Mkristo." Namba 7 na 8 zinafanya kazi

katika

maisha

haya,

namba

9

hufanyika mwishoni mwa maisha haya, na namba 10 hufanyika wakati Kristo anarudi. Ninachoweza

kusema

hapa

ni

kwamba

hakuna mwenye makosa katika mipangilio hiyo. Mambo yote waliyoainisha yanatukia 33

katika maisha ya wokovu wa mwanadamu ingawa hatuwezi kujua ni lini na katika hali gani.

SURA YA TATU KUCHAGULIWA MAPEMA NA KUITWA a. Kuchaguliwa Kwa sababu wale aliowajua tangu asili, aliwachagua

tangu

awali,

afanane

na

mfano wa Mwanawe, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza kati ya ndugu wengi. na wale aliowateua aliwaita;

na

tangu

mwanzo,

hao

pia

wale

aliowaita,

hao

pia

aliwatangaza kuwa waadilifu. na wale 34

aliowatangaza kuwa waadilifu, hao pia aliwatukuza.15 Wanazuoni wa Kirefomati na wale wa Kimatengenezo

wanakubaliana

kuhusu

hatua hii ya mwanzo kabisa ya wokovu wa mwanadamu. Ni mojawapo ya hoja muhimu sana katika soteriolojia ya Kibiblia kwa sababu

usipoelewa

“kuchaguliwa unaweza mingine, kujikuta

mapema”

kushindwa na

vizuri basi

yamkini

kuelewa michakato

matokeo

umeingia

kuhusu

yake

katika

unaweza

mikanganyiko

mikubwa.” Kabla hatujaendelea ningependa kukushauri chochote sababu

tu

kwamba, kuhusu

mafundisho

usisome

kitabu

“soteriolojia” ya

kwa

Arminianism16

Tafsiri yangu kutoka “Young Literal Translation Bible.” Arminianism ni tawi la Uprotestanti linalotegemea maoni ya kiteolojia ya mwanateolojia wa Uholanzi Jacobus Arminius (1560-1609) na wafuasi wake wa kihistoria wanaojulikana kama Remonstrants. 15 16

35

yametapakaa nitakuwa

makanisani.

sahihi

mafundisho

Huenda

nikisema

mengi

kwamba

ambayo

huwa

ninayasikia makanisani kuhusu wokovu yameegemea

kwenye

Arminianism.

Sitakuwa

kujadili

upinzani

mlengo na

wa

wa

muda

wa

Arminianism

kihistoria. Katika

Maandiko

Matakatifu

kuna

maeneo mengi ambayo yanaonyesha Mungu aliwachagua watu kwa kazi fulani au kazi maalumu. Kwa mfano aliwachagua watu kwa

ajili

ya

uongozi

maalumu,

mfano

alivyomchagua Musa kuwaongoza wana wa Israeli, huu nao ulikuwa ni uchaguzi wa Mungu 2:23).

(Hes. Vilevile

16:5-7), Mungu

Zerubabeli,

(Hag.

alichagua

kabila

fulani kwa ajili ya kazi maalumu, kwa ajili ya huduma fulani. 36

Tunapokuja kwenye Agano Jipya, tuna maandiko mengi sana ambayo yanaonyesha kwamba Mungu amewachagua watu kwa ajili ya wokovu. WCF/3/2/ inasema “ili kudhihirisha

utukufu

wake,

Mungu

amewachagua watu wengine (na malaika) kwa uzima wa milele na kwamba wengine amewachagua kwa kifo cha milele.” (1 Tim 5:21, Mt 25:31,41, Mdo 13:48, Rum 8:2930, Yn 10:27-29, Mk 8:38, Yud 6. Rum 9:22-23, Efe. 1:5-6, Mith 16:4, Mt 25:41, Yud 4). Fundisho

hili

kuchaguliwa”

(kwa

predestination) mstakabari mbinguni

linaitwa

ambapo

wetu ama

wa

“kutangulia kiingereza,

Mungu

aliamua

maisha;

kwenda

kuzimu

hata

kabla

hatujazaliwa. Mungu amechagua wengine kuokolewa, na wengine ameruhusu kuvuna 37

matokeo ya dhambi zao. Huu ni uchaguzi usio na masharti; kwa maana ya kwamba anayechaguliwa hajafanya jambo lolote lile la kumpendeza Mungu, bali Mungu, kwa hiari yake mwenyewe bila kulazimishwa na matendo ya mtu anayechaguliwa. Mara nyingi

udhihirisho

wa

uchaguzi

huu

hujidhihirisha kwa njia ya huduma ya Roho Mtakatifu

kupitia

Neno

la

Mungu

linalohubiriwa. Wale

ambao

wamechaguliwa,

si

kwamba wamechaguliwa kwa sababu ya imani yao, na wala si kwa sababu ya matendo

yao

kwamba

Mungu

amewachagua, bali ni kwa sababu ya uhuru wake mwenyewe kwa jinsi alivyoamua bila kuingiliwa na kiumbe ambacho amekiumba. Katika hili wengi huuliza “imani” ina kazi gani sasa? Ama kwa hakika imani ni 38

matokeo ya uchaguzi wa Mungu ambao hautegemei mwenyewe. kisoteriolojia

mwanadamu, Katika

bali

Mungu

muktadha

tunamwamini

Kristo

wa kama

matokeo ya kile ambacho Kristo amekifanya katika maisha yetu. Uchaguzi wa Mungu kwa ajili ya wokovu ni “uchaguzi usio na vigezo”

(unconditional

election).

Warumi

9:10-13 inasema: Wala si hivyo tu, lakini Rebeka naye, akiisha kuchukua mimba kwa mume mmoja, naye ni Isaka, baba yetu, (kwa maana kabla hawajazaliwa

wale

watoto,

wala

hawajatenda neno jema wala baya, ili lisimame kusudi la Mungu la kuchagua, si kwa sababu ya matendo, bali kwa sababu ya nia yake aitaye), aliambiwa hivi, Mkubwa atamtumikia mdogo. Kama ilivyoandikwa,

39

Nimempenda

Yakobo,

bali

Esau

nimemchukia. Ingawa wote wawili Yakobo na Esau walikuwa wazao wa asili wa Isaka, Mungu aliwatendea mdogo

tofauti

kuliko

kwa

mkubwa.

kumpendelea Uamuzi

huu

haukutegemea "chochote kizuri au kibaya" ambacho

walikuwa

wamefanya,

lakini

ilikuwa ili kusudi la Mungu katika uchaguzi lisimame.

Chaguo

hilo

halikuwa

na

masharti, ikimaanisha kwamba haikuwa kwa matendo ilikuwa kwa Yeye mwenye kuita. Yakobo alipendelewa kwa sababu ya mapenzi makuu ya Mungu, sio kwa sababu ya kitu ambacho alikuwa amefanya au angefanya; Chaguo la Mungu lilikuwa huru kabisa. Luther anasema kwamba, “Mungu anaona mapema, anakusudia, na hufanya vitu vyote kulingana na mapenzi Yake 40

yasiyoweza kubadilika, ya milele na yasiyo na makosa."17 Katika "Maana yeye

Warumi

amwambia

Musa,

nimrehemuye,

nimhurumiaye.” hitimisho

9:15

tunasoma, Nitamrehemu

nitamhurumia

Mstari

wa

linalodhihirisha

16

yeye

unatoa

mamlaka

ya

Mungu ya kuchagua, “Basi, kama ni hivyo, si katika uwezo wa yule atakaye, wala wa yule apigaye mbio; bali wa yule arehemuye, yaani, Mungu.” Paulo anasema kwamba Mungu alituokoa kwa sababu ya kusudi na neema yake mwenyewe, sio kwa sababu yoyote wala hali yoyote ambayo aliona ndani yetu. Fundisho

hili

halitoki

kwa

John

Calvin, kama wapinzani wa fundisho hili Martin Luther, The Bondage of the Will; (Grand Rapids, Michigan: Fleming H. Revell, 2000) 80. 17

41

wanavyodai, bali linatoka kwenye Biblia. Neno "tangu asili aliwachagua” ndiyo haswa “kutangulia

kuchaguliwa"

linapatikana

katika Warumi 8: 29,30 na Waefeso 1: 5,11. Maneno

"wateule"

na

"uchaguzi"

yametumika mara 14 katika Agano Jipya. Wazo la udhibiti wa Mungu kuhusu wokovu wa

wenye

dhambi

linapatikana

katika

vifungu mbalimbali vya Biblia (Mt. 24:22; Mk. 13:27; Rum. 11: 7; II Tim. 2:10; Tito 1: 1; 1 Petro 1: 1; Mdo. 13:48; Yoh.6:37; 10: 27-29; 6:39, 44, 65; (17: 6,9) Dhana potofu kuhusu kuchaguliwa mapema Fundisho hili “kiwepesi sana limekuwa halieleweki

na

linapotoshwa.18

Nitaweka

hoja nne ambazo wapotoshaji wa fundisho hili hudai. 18

Mayhue uk. 505

42

Kwanza,

wanaopinga

fundisho

hili

hudai kwamba kutangalia kuchaguliwa ni “hatma

isiyowajibisha”

(kiingereza

fatalism). Wapotoshaji husema kwamba watu wengine wanataka kuja kwa Yesu lakini

hawawezi

hawajachaguliwa

kwa

sababu

mapema.

Sentensi

mashuhuri inayotumika ni hii "Unaweza, lakini huwezi, utaweza lakini hutafanya hivyo, utahukumiwa ukifanya hivyo, na utahukumiwa ikiwa hutafanya hivyo.” Pili, wanadai kwamba, kama Mungu amewachagua watu wengine kwa uzima wa milele na wengine kwa hukumu ya milele, basi mwenye shida ni yule anayechagua; kwani mchaguliwa hana tatizo lolote. Tatu, ikiwa ni hivyo, basi, hatuhitaji kuhubiri

Injili

ameshachagua

kwa walio 43

sababu wake;

hata

Mungu kama

tukihubiri

haiwezi

kubadilisha

kitu

chochote. Nne, vilevile

ikiwa ni hivyo, basi,

hatuhitaji hata kuomba kwa ajili ya watu ambao hawajaokolewa kwa sababu maombi yetu hayawezi kubadilisha kusudi la Mungu la tangu asili. Majibu kwa dhana potofu Kuchaguliwa

mapema

kamwe

hakuwezi kufuta jukumu la kibinadamu. Waislamu husisitiza “majaliwa ya Mwenyezi Mungu.” Fundisho la majaliwa ya Mungu huondoa

wajibu

kuweka

wajibu

kwa

mwanadamu,

wote

kwa

na

Mungu.

kuchaguliwa mapema haifundishi hivyo, watu

wote

wanapaswa

kuwajibika

dhambi na makosa yao yote.

44

kwa

Pia,

kuchaguliwa

mapema

haifuti

mwito wa watu wote kuitikia Injili na kwamba wajibu wa mwanadamu ni kufanya kile ambacho Mungu ameagiza.

Wito wa

Mungu ni kwa watu wote. (Mt. 11:28). Upendo wa Mungu ni kwa watu wote. (Yn. 3:16). Watu wote wanapaswa kutubu. (Mdo. 17:30). Kuna ahadi kwa wale wanaotii. (Rum 10:13). Maagizo na ahadi za Mungu yanayopatikana katika Maandiko yanabaki palepale

na

mapema.

Katika

tunaangalia

hayatangui

kuchaguliwa

kuchaguliwa

hasa

mapema,

kile ambacho

Mungu

alifanya, amefanya na atafanya kwa maisha ya

mwanadamu;

mwanadamu

na

si

alifanya,

kile

ambacho

amefanya

na

atafanya kwa ajili ya Mungu. Fundisho

hili

linaegemea

kwenye

uhuru wa Mungu wa kufanya kila kitu 45

apendacho kwa wakati wake; na pia wajibu wa mwanadamu hautanguki kwa sababu ya uhuru

wa

Mungu.

Tunakiri

kwamba

fundisho la kuchaguliwa mapema ni gumu kueleweka,

lakini

halifundishwi

na

haimaanishi Biblia.

Si

kwamba kila

kitu

tunaweza kuelewa katika Biblia, bali kwa sehemu tu tunaweza kuelewa. Ni Wateule tu Tunapaswa

kuwa

makini

tunapozungumzia hoja hii ili kutokuleta mkanganyiko kwa wengine. Ninachoweza kubainisha

mapema

hapa

ni

kwamba

wokovu siyo kwa watu wote, ni kwa wateule tu, kwa sababu kamwe dhabihu ya Kristo haiwezi

kufanyika

Vilevile,

hatukubaliani

kwamba

pasipo

wanadamu

na wote

na

ufanisi.

mawazo

ya

wataokolewa

mwishoni (universal salvation) kwa sababu 46

ingekuwa

hivyo,

basi

watu

wengine

wasingefia dhambini. Kwa hiyo wokovu unathibitiwa kwa idadi maalumu ya watu. Kwa hiyo ni sahihi kusema kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya Wateule, si watu wote. Najua unaweza kushangaa! Biblia inasema, “kwa maana mwana wa Adamu naye hakuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya WENGI” (Mk. 10:45). Angalia neno hilo, fidia kwa wengi siyo kwa WOTE. Wanaookolewa ni wengi sana sana, lakini pia watu wanaofia dhambini na watahukumiwa adhabu ni wengi. Tunasoma katika WCF/3/5 kwamba, Mungu,

kabla

hata

ya

kuumba

ulimwengu, kulingana na mpango wake wa milele, usiobadilika, na kusudi lililofichika na

mapenzi

yake

mema

amewachagua

baadhi ya wanadamu katika Kristo, ambao 47

amewaamuru kwa uzima na utukufu wa milele.

Amefanya

hili

kwa

rehema

na

upendo wake na kwa sifa ya neema yake ya ajabu, alifanya uchaguzi huu kwa uhuru wake

mwenyewe,

kwa

jinsi

alivyotaka

viumbe vyake viwe. Uteuzi huu hautegemei imani yao au matendo mema au uvumilivu wao,

bali

inategemea

yeye

mwenyewe

Mungu katika uchaguzi wake. Efe. 1:4, 9, 11, 2Tim 1:9, Rum 8:30, 1Thes 5:9, 1 Pet 5:10 Efe. 1:5-6, 12 Rum 9:11, 13, 15-16, Efe. 1:4,6,9, 2 Tim 1:9, Efe. 2:8-9). Katika sehemu inayofuatia, WCF/3/6 inasema, Kwa kuwa Mungu ameamuru Wateule watukuzwe katika yeye, vivyo hivyo, katika kusudi lake la milele na huru kabisa la mapenzi yake, amepanga namna ambavyo uchaguzi huo unatimizwa. Na hivyo, wale 48

waliochaguliwa, katika

wakiwa

Adamu,

wameanguka

wamekombolewa

katika

Kristo. Wameitwa kwa imani kwa Kristo na Roho wake anafanya kazi ndani yao kwa wakati unaofaa, na wamehesabiwa haki, wamefanywa

wana,

wamehifadhiwa

wametakaswa,

na

nguvu

zake

na

kupitia

imani kwa ajili ya Wokovu, Ni Wateule tu, na hakuna

wengine,

wanaokombolewa

na

Kristo, wanaoitwa, wanaohesabiwa haki, wanaofanywa

wana,

wanaotakaswa,

na

wanaookolewa.” Mungu, kulingana na makusudi ya siri ya mapenzi yake mwenyewe, ambayo yeye hutoa au huzuia rehema kwa utukufu wa uweza wake wa kutawala juu ya viumbe vyake, ilimpendeza kutowaita baadhi ya watu wengine na kuwaweka kwa uharibifu na hasira kwa dhambi zao kwa sifa ya haki 49

yake tukufu. Kwa hiyo “maamuzi ya Mungu ni

kutokuwachagua

wengine

na

hivyo

kuwaacha katika uangamivu wa dhambi zao.19 Haishangazi

kuona

kwamba

kuna

idadi maalumu ya watu ambao wataokolewa kwa sababu Mungu ndiye ambaye anajua kila kitu, na kwa hivyo hata watu ambao hatawaokolewa tayari Mungu amekwisha panga. 1 Pet. 2:8b inasema, “wasiliamini nao waliwekwa kusudi wapate hayo.” Watu Mungu,

ambao

hawakuchaguliwa

wanaendelea

na

kufanya

yanayomchukiza Mungu ili wapate hukumu ya haki. Yuda 4 inasema, “Kwa maana kuna watu

waliojiingiza

kwa

siri,

watu

walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, Macarthur J & Mayhue, R (Ed) A Systematic Summary of Biblical Truth: Biblical Doctrine (Wheaton, Illinois: Crossway, 2017) uk. 504 19

50

makafiri, wabadilio neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi, nao humkana yeye aliye peke yake Mola, na Bwana wetu Yesu Kristo.” Kwa maelezo haya, ningependa kusisitiza kwamba ni dhahiri kabisa kwamba kuna watu ambao Mungu amewakataa, yaani hajawachagua. Grudem anatupa ufafanuzi katika hili kwamba, “amri ya kukataliwa ni chaguo huru la Mungu, lililofanywa katika umilele

uliopita

akichagua

kutoweka

upendo wake wa kuokoa juu yao lakini badala yake akiamua kuwaadhibu kwa dhambi zao...”20 WCF/3/8

inamalizia

kwa

kusema

kwamba, “fundisho hili muhimu na la kushangaza

la

kuchaguliwa

na

Mungu

lazima lishughulikiwe kwa busara sana, ili

Wayne Grudem, Systematic Theology (Grand Rapids: MI: Inter-Varsity Press 1994),678. 20

51

kutii mapenzi ya Mungu yaliyofunuliwa katika neno lake, watu wengine wanaweza kuwa

na

hakika

kuwa

wamechaguliwa

milele kutoka kwa ukweli wa wito wao wenye ufanisi. Kwa njia hii, fundisho la uchaguzi wa Mungu

litazidi kuwafanya

watu wamsifu Mungu na kuendelea kuwa wanyenyevu na kutii Injili.” Kwa fundisho

yeyote

ambaye

ameshaelewa

hili na kupokea moyoni kwa

kuamini kwamba wokovu wake si kwa sababu yake mwenyewe, bali Mungu pekee amemteua kwa ajili ya kupokea wokovu huo,

basi

atakuwa

na

sababu

ya

kumshukuru Mungu, na kuwa mtu mwenye wivu zaidi kwa ajili ya kazi ya Mungu. Hata hivyo,

kwa

fundisho

yeyote hili,

ambaye anaweza

hajaelewa kujikuta

ametumbukia kwenye maisha ya dhambi 52

yasiyo na mfano, na ikionekana hivyo, moja kwa moja ataonesha wazi dalili za kuwa mwana wa upotevu. Kwa chochote

hiyo,

fundisho

kile

ambacho

hili

haliondoi

mwanadamu

anapaswa kufanya katika maisha haya kama

kilivyofunuliwa

katika

Maandiko

Matakatifu; Hakuna mwanya wa kuacha kuhubiri Injili kwa kigezo cha kwamba Mungu amechagua baadhi na kuwaacha baadhi. Kile ambacho Mungu ameagiza katika Maandiko kifanywe. Wakati wote tunapaswa

kutii

kile

ambacho

Mungu

amesema katika neno lake hata kama usipojua sababu za kutii kwake. Hata

hiyo,

tunahubiri

Injili

kama

mwito wa kuwakusanya wateule wa Mungu, sisi hatujui ni nani mteule Yesu alisema, “Kwa maana waitwao ni wengi, bali wateule 53

ni wachache.” (Mat. 22:14). Tunapohubiri ndipo wateule wanaitikia mwito wao. Mungu anavumilia matukio kadhaa kwa ajili ya kuwaokoa

wateule,

“Na

kama

Bwana

asingalizikatiza siku hizo, asingeokoka mtu ye

yote;

lakini

kwa

ajili

ya

wateule

aliowateua amezikatiza siku hizo.” (Mk. 13:20) Maswali fikirishi 1. Je

kuchaguliwa

kunakusaidiaje

mapema

wewe

kutambua

wokovu wako? 2. Je kuna uhusiano gani kati ya “kuchaguliwa

mapema”

“kushikilia

wokovu

na usije

ukakuponyoka.”? 3. Unafikiri kwa nini fundisho hili, pamoja

na

kuwa

54

linafundishwa

vizuri

katika

Biblia

watu

wengi

wanashindwa kuelewa? b. Kuitwa Warumi mchakato

8:30 wa

inatuelekeza kuitwa,

kwenye

“Na

wale

aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, hao akawahesabia haki; na

wale

aliowahesabia

haki,

hao

akawatukuza.” Mara nyingi wito huu huitwa “wito wenye ufanisi” (effectual calling).

Katika

maisha ya kawaida tunasema kwamba mtu akiitwa

lazima

aitike,

kama

asipoitika

maana yake wito utampita. Hata hivyo, kama lilivyo jina lake kwamba “wito wenye ufanisi”

hakuna

namna

yoyote

ya

kupingana nao, kwa sababu ni wito wenye ufanisi.

Sinclair

B.

Ferguson

anasema

kwamba “kwa kuwa wito wenye ufanisi ni 55

ule ambao matokeo yake yamehakikishwa, sio

kama

"mwaliko"

kwamba

wateule

wanaweza kukubali au kukataa.”21 Grudem anaongezea kwamba “Wito huu wito ni aina ya "wito" kutoka kwa Mfalme wa ulimwengu na una nguvu ambayo inaleta majibu katika mioyo ya watu.”22 John Frame anasema kwamba wakati mwingine wito humaanisha tangazo la injili kwa wote, ambapo Mungu huita au hualika kila mtu amwamini Kristo na kuokolewa (Mt. 20:16; 22:14). Huo wakati mwingine huitwa wito wa injili au wito wa nje. Hayo pia ni mafundisho muhimu ya kibiblia. Lakini sio maana ya wito wenye ufanisi.23 Katika wito wenye ufanisi Mungu hufanya Vincent Cheung, Systematic Theology. 190. Wayne Grudem, Systematic Theology (Grand Rapids: MI: Inter-Varsity Press 1994),961. 23 John M. Frame, Salvation Belongs to the Lord: An Introduction to Systematic Theology (New Jersey: P & R Publishing, 2006), 123. 21 22

56

kwanza

kwetu

kabla

ya

sisi

kuitikia

chochote.24 Sinclair Ferguson anafafanua kwamba, "Yeye anayewaita huunda ndani yao uwezo wa kuitikia ili kwamba katika kitendo cha wito

wake

huwaingiza

katika

maisha

mapya."25 Katika WCF/10/1 tunasoma kwamba, “Mungu huwaita kwa wakati unaofaa wale tu ambao yeye amewaandaa kwa uzima wa milele. Anawaita kwa Neno lake na Roho wake kutoka kwenye hali yao ya asili ya dhambi na kifo ili kuingia katika neema na wokovu kupitia Yesu Kristo. Anawaangazia katika akili zao za kiroho uelewa uokoao wa vitu vya Mungu. Anaondoa mioyo yao ya John M. Frame, Salvation Belongs to the Lord: An Introduction to Systematic Theology. 124. 25 Sinclair B. Ferguson, The Christian Life: A Doctrinal Introduction (Carlisle, Pennsylvania: The Banner of Truth Trust, 1997), 34. 24

57

mawe na huwapa mioyo ya nyama. Yeye huboresha mapenzi yao kwa uweza wake uwezao kuwaongoza kwa yaliyo mema. Na kwa hiyo anawavutia kwa Yesu Kristo. Lakini wanakuja kwa Yesu kwa hiari yao wenyewe,

wakiwezeshwa

na

neema

ya

Mungu. Swali hapa tunalopaswa kujiuliza ni je Mungu

hutoa

wito

wake

kwa

kulenga

wateule tu, au hata watu wengine wasio wateule? Katika kujibu swali hili tunahitaji kujua kwanza ni kwa namna gani Mungu hufanya wito wake na wakati gani. Mungu hutoa wito wake kwa njia ya Neno lake, kwa njia ya mahubiri. Mungu huwaita wateule kawaida kwa njia ya kuhubiri injili. Injili haihubiriwi kwa wateule tu, bali ni kwa kila kiumbe

“Akawaambia,

Enendeni

ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa 58

kila

kiumbe.

ataokoka;

Aaminiye

asiyeamini,

na

kubatizwa

atahukumiwa.

"(Marko 16: 15-16). Kwa hivyo, iwe ni kwa njia ya mahubiri ya mikutano ya Injili, mazungumzo ya kibinafsi, au kwa kusoma vitabu vya kidini na kuguswa na kuweza kuja kwa Kristo. Wito wenye ufanisi ni kwa Wateule tu, ingawa

hata

wale

ambao

si

wateule

wanaweza kuja kwenye nuru kupitia wito wa ujumla. Tunasoma ufafanuzi katika WCF/10/4

kwamba,

“Wengine,

wasio

Wateule, wanaweza kuitwa na huduma ya Neno, na Roho anaweza kufanya kazi ndani yao kwa njia ambazo hufanya kwa Wateule. Walakini, kamwe hawatakuja kwa Kristo na kwa hiyo hawawezi kuokolewa. Katika 1 Yohana 2:19 tunasoma kwamba, “Walitoka kwetu, lakini hawakuwa wa kwetu. Maana 59

kama wangalikuwa wa kwetu, wangalikaa pamoja nasi. Lakini walitoka ili wafunuliwe kwamba si wote walio wa kwetu.” Katika fungu hili, “hawakuwa wa kwetu” maana yake ni watu waliosikia Injili wakaitikia lakini kwa sababu si wateule hawakuweza kuendelea. Na kwa kweli, watu bila kumkiri Kristo

hawawezi

kuokolewa

kwa

njia

nyingine yoyote; Maandiko yanasema, “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.” (Mdo. 4:12) haijalishi wanajaribu sana kuishi maisha ya maadili kulingana na uelewa wao wenyewe au kujaribu kufuata sheria za dini nyingine. Kwa hiyo ile dhana iliyozoeleka kwamba “wokovu ni matendo yako” haifai kwa lolote 60

kwa sababu wokovu unapatikana kupitia Kristo peke yake. Ukisema kwamba “wokovu ni matendo tu” jiulize pia kwamba je, Mungu anafaikaje na matendo yako mema (haimaanishi kwamba matendo mema si muhimu, lakini si muhimu kwa kupata wokovu) Wanateolojia

wengine

hutofautisha

kati ya “wito wa nje” na “wito wa ndani” kwa maelezo kwamba wito wa nje unahusu mahubiri ya injili kwa wanadamu wote; kwa wateule na wasio wateule. Wito wa ndani au ambao ndio huitwa “wito wenye ufanisi” ni kazi ya Mungu inayoambatana na wito wa nje ili kusababisha wateule kuja kwenye imani katika Kristo. Kuhubiriwa kwa injili inaonekana kama wito wa nje kwa watu wote, lakini pia inakuwa wito wa ndani kwa wateule. Wito wa nje hutolewa na wahubiri, 61

lakini wito wa ndani ni kazi ya Mungu ambayo hufanyika kwa wateule tu. Na wito huu

wa

ndani

kwa

kawaida

huenda

sambamba na wito wa nje. Kwa maneno mengine, watu “wengi wanaweza kusikia injili katika mazingira fulani, lakini Mungu atasababisha

wateule

tu

kuamini

kile

kinachohubiriwa, wakati huo pia anafanya wagumu wasio wateule dhidi yake.”26 Wito wa nje ambayo ndiyo mahubiri ya umma ni ya muhimu sana kwa sababu pasipo kusikia neno la Mungu hatuwezi kuja kwenye wito wetu. (Rum. 10: 14). Ni njia ya kawaida ambayo Mungu ameichagua kuwatumia watumishi wake kwa ajili ya kuwaita wateule wengine kupokea wokovu wao.

26

Vincent Cheung, Systematic Theology. 191.

62

Wito

wenye

ufanisi

unatuita

sisi

kushiriki katika baraka zote za wokovu: ufalme (1Thes. 2:12), utakatifu (Rum. 1: 7; 1 Kor. 1: 2; 1 The. 4: 7), amani (1 Kor. 7:15), uhuru (Gal. 5:13), tumaini (Efe. 1:18), subira (1 Petro 2: 20-21), uzima wa milele (1 Tim.

6:12).

Mwishowe,

wito

ni

katika

ushirika na Kristo, umoja na Kristo; 1 Wakorintho 1: 9 inasomeka, “Mungu ni mwaminifu ambaye mliitwa na yeye mwingie katika ushirika wa Mwanawe, Yesu Kristo Bwana wetu.” Baraka ya wokovu ni Kristo mwenyewe, na kila kitu yeye hufanya kwa niaba yetu; Kwa hiyo, Paulo anasema katika Wafilipi 3: 7-8, " Lakini

mambo

yale

yaliyokuwa

faida

kwangu, naliyahesabu kuwa hasara kwa ajili

ya

Kristo.

Naam,

zaidi

ya

hayo,

nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa 63

ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata

hasara

ya

mambo

yote

nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nipate Kristo;” Je Mungu hawalazimisha Wateule Kuitikia Wito? Ingawa wengi wanakataa utashi huru wa

mwanadamu,

kwamba

“Mungu

WCF/9/1 amempa

inafafanua mwanadamu

utashi, ambao kwa asili ni utashi huru, yaani

sio

wa

kulazimishwa

au

lazima

kuelekea mema au mabaya (Mt 17:12, Yak. 1:14, Kumb. 30:19, Yn 5:40, 7:17, Ufu 22:17, Mdo 7:51, Yak 4:7.)” Kwa misingi hiyo, Mungu hamlazimishi mwanadamu, bali

hulainisha

utashi

wake

ili

aweze

kupokea au kutokupokea Injili. Kwa hiyo si sahihi

kusema

kwamba 64

Wateule

wanalazimishwa

kuitikia

mwito,

bali

“wanawezeshwa” kuitikia. Katika Yohana 6:44 tunasoma, “Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka; nami nitamfufua siku ya mwisho.” Kupitia

Injili

Mungu

hutuambia

katika ukamilifu wa ubinadamu wetu. Kwa kuwa sisi ni wateule, lakini Mungu hatuokoi kama “roboti” bali “kutafuta jibu kutoka kwetu kama watu wazima, kupitia akili zetu,

hisia

zetu,

na

mapenzi

yetu.

Anazungumza na akili zetu kwa kuelezea ukweli

wa

wokovu

katika

Neno

lake.

Anazungumza na mihemko yetu kwa kutoa mwaliko wa kibinafsi, anazungumza na mapenzi

yetu

kwa

kutuuliza

kututaka

kuitikia mwaliko wake kwa hiari yetu.”27

27

Wayne Grudem, Systematic Theology. 964.

65

Kwa

hiyo,

tunaitwa

kupitia

neno

linahubiriwa, na wakati huo Roho Mtakatifu hufanya kazi ya kutufanya kujua dhambi zetu na kutufanya kupokea kwa hiari wito wa

Mungu.

Wakati

mwingine

Mungu

ametumia mazingira kadhaa kwa ajili ya kuwaita wateule; kwa mfano kuna watu ambao walikuwa katika Uislamu, ambao walisoma Biblia peke yao na kugundua ukweli wa Biblia. Wengine walipookoka walisema

kwamba

walitokewa

na

Yesu

Kristo katika ndoto, kwa hiyo hawawezi kupingana na wito wake. Maswali fikirishi 1. Vipi kuhusu watu ambao hawawezi kuonesha mwitikio wao wa wito wao wa nje, na mwishowe wanakufa bila kuonyesha

mwitikio?

66

Kwa

mfano

watoto, au wagonjwa mahututi? Nini ufafanuzi wako kwenye hili? 2. Kama

wokovu

unapatikana

katika

Kristo peke yake, je watu wa Agano la Kale waliokolewaje? Rejea (WCF/8/4)

SURA YA NNE

67

KUZALIWA UPYA NA KUHESABIWA HAKI

a. Kuzaliwa Upya Maana ya kuzaliwa upya: tunahitaji ufafanuzi wa kutosha kuhusu maana ya kuzaliwa upya. Wayne Grudem anasema kwamba, ni “neno la kimaandiko (Yohana 3: 3-8) likimaanisha kazi ya Mungu ambayo kwayo

anatupatia

maisha

mapya

ya

kiroho.”28 Grudem anasema kwamba ni tendo la siri la Mungu, na wakati mwingine huitwa “regeneration.”29 Ni tendo la siri la Mungu kwa sababu linafanyika bila sisi kujua kitu chochote, ni kazi

ambayo

Roho

Mtakatifu

huifanya

katika maisha ya Wateule. Kwa kweli, hakuna jukumu lolote ambalo mwanadamu 28 29

Wayne Grudem, Systematic Theology. 964. Wayne Grudem, Systematic Theology. 670.

68

anaweza kufanya katika tendo la kuzaliwa mara

ya

pili.

kunatangulia

Kuzaliwa kuitwa,

mara

kwa

ya

pili

maana

ya

kwamba mtu hawezi kupokea wito wenye ufanisi ikiwa hajazaliwa mara ya pili. Kwa maneno

mengine

“kuzaliwa

upya”

haimaanishi uongofu kwa ujumla, bali ni ile kazi ya ndani ya Roho Mtakatifu kwa maisha

ya

wateule.

Cheung

anasema

kwamba, “Kuzaliwa upya, au "kuzaliwa mara ya pili," hufanyika kwa kushirikiana na wito wa Mungu kwa wateule wake (1 Petro 1:23; Yakobo 1:18), na huwawezesha kumpokea Kristo kwa imani na toba. Hii inamaanisha

kuwa

kuzaliwa

upya

hutangulia imani; yaani mtu hazaliwi mara ya pili kwa imani, lakini amewezeshwa kuamini

kwa

amemfanya

sababu

upya.

Imani 69

Mungu sio

tayari

sharti

la

kuzaliwa upya; badala yake, kuzaliwa upya ni

sharti

ya

imani.

Sababu

kwa

nini

Wakristo wengine kufikiria kuwa kuzaliwa upya hutokea kwa imani ni kwa kwamba huchanganya maana ya “kuzaliwa upya” na “wokovu” Neno "wokovu" linapotumiwa kwa mwenye dhambi, ni neno la kawaida ambalo linamaanisha idadi ya mambo mengi.”30 Kama

ambavyo

tumejifunza

hapo

nyuma kwamba Mungu amechagua watu kadhaa kwa ajili ya kupokea wokovu. Kristo alikuja duniani kwa ajili ya kulipa la dhambi kwa hawa wateule. Kwa hiyo, ila mteule ameitwa kuamini injili kwa nyakati maalum zilizowekwa na Mungu. Walakini, kwa

kuwa

wateule

wamezaliwa

wenye

dhambi, ndani yao kuna mwelekeo wenye nguvu kuelekea uovu, ambao huwafanya 30

Vincent Cheung, Systematic Theology. 192.

70

wasiweze kuitikia mwito wao, kwa hiyo, Mungu kufanywa upya wenye dhambi na kuwaita. Katika

kuzaliwa

upya,

moyo

wa

mwanadamu hufanywa mwepesi kupokea mapenzi ya Mungu na kuamini neno lake. Biblia inasema habari ya kuokolewa kwa mwanamke mmoja aliyeitwa Lidya. Inasema kwamba

“Mwanamke

mmoja,

jina

lake

Lidia, mwenye kuuza rangi ya zambarau, mwenyeji

wa

akatusikiliza,

Thiatira, ambaye

mcha

Mungu,

moyo

wake

ulifunguliwa na Bwana, ayatunze maneno yaliyonenwa na Paulo.” (Mdo 16:14) Katika kuzaliwa upya, Roho Mtakatifu, “kupitia mahubiri ya Injili huweka uzima wa kiroho kwa mwenye dhambi, akimtoa

71

kutoka kwenye kifo cha kiroho na kumwingiza katika uzima wa kiroho.”31 Yakobo 1:18 inasema, “Kwa kupenda kwake mwenyewe alituzaa sisi kwa neno la kweli, tuwe kama limbuko la viumbe vyake.” Yesu Kristo anatuonyesha jinsi ya kuzaliwa mara ya pili. Katika Yohana 3:3 Yesu anaonyesha umuhimu wa kuzaliwa mara ya pili, “Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.” Katika Mstari wa 7-8 anasem, “Usistaajabu kwa

kuwa

nilikuambia,

Hamna

budi

kuzaliwa mara ya pili. Upepo huvuma upendako, na sauti yake waisikia, lakini hujui

unakotoka

wala

unakokwenda;

kadhalika na hali yake kila mtu aliyezaliwa Macarthur J & Mayhue, R (Ed) A Systematic Summary of Biblical Truth: Biblical Doctrine. 585. 31

72

kwa Roho.” Yesu hapa anaonyesha namna tukio

la

kuzaliwa

linavyofanyika, kuonekana

mara

kama

kwa

ya

upepo;

macho,

pili

haliwezi

hata

hivyo

tunaweza kuona matokeo yake. Matokeo ya kuzaliwa mara ya pili ni mtu kupokea Injili, kumpokea Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi

wa

maisha

yake.

Nikodemo

hakuelewa, kwa hiyo anauliza katika mstari wa 9, “Nikodemo akajibu, akamwambia, Yawezaje kuwa mambo haya?” Aliona ni mambo ambayo hayawezekani hata kidogo, lakini

Yesu

yanawezekana.

alimwambia Ni

jambo

kwamba la

kiroho,

linalofanywa na Roho Mtakatifu. Matokeo ya wazi kabisa ya kuzaliwa mara ya pili ni kuonyesha matunda ya Roho Mtakatifu, kwa sababu umezaliwa upya. Kwa hiyo ni muhimu matunda ya Roho 73

Mtakatifu

yaonekane,

akiendelea

kufanya

vinginevyo maovu

mtu

yamkini

atakuwa bado hajazaliwa mara ya pili, kwa hiyo ana wokovu feki. Paulo anatusaidia kutambua matunda hayo; “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.” (Gal. 5:22-23), na Yesu alibainisha wazi kwamba “Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti? Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya. Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri. Kila

mti

usiozaa

tunda

zuri

hukatwa

ukatupwa motoni. Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua.(Mat. 7:16-20) 74

Maswali fikirishi 1. Je

kuna

ufahamu

mpya

kuhusu

“kuzaliwa mara ya pili” tofauti na ule uliousikia kwenye mahubiri ya Injili? 2. Ni kwa vipi mwanadamu anaweza kushiriki katika “kuzaliwa upya?” 3. Je kuna uwezekano wale waliozaliwa upya wakashindwa kuitikia mwito? b. Kuhesabiwa Haki Wanazuoni wanatofautiana kimpangilio na matumizi ya maneno kuhusu hatua hii. Kwa mfano Wayne Grudem anatumia neno, “Uongofu (imani na toba.)”32 Frame yeye anatumia “imani na toba.”33 Vincent Cheung anatumia neno “kuongoka.”34 Mpangilio wa Macarthur J & Mayhue, unaonesha Wayne Grudem, Systematic Theology. 978. John M. Frame, Salvation Belongs to the Lord: An Introduction to Systematic Theology. 127. 34 Vincent Cheung, Systematic Theology. 193. 32 33

75

kwamba baada ya Kuzaliwa Upya inakuja, “toba.”35 Kwa kuwa hawajafafanua kwa nini wamepangilia hivyo, ni vigumu kujadili mpangilio wao.

Herman Bavinck naye

anatumia neno, “Imani na uongofu.”36 Nisingependa kujadili kwa undani sana tofauti hizo, lakini ninachoweza kusema hapa

ni

kwamba

mambo

yote

haya

yanapatikana katika wokovu. Ili kutatua tofauti ya maneno haya tutatumia neno “kuhesabiwa haki” kama tulivyobainisha kwenye kichwa hicho. Maneno

yanayohusiana

“kuhesabiwa

haki”

ni

na pamoja

neno na

“kuhesabiwa haki kwa imani” au “kuwa na haki. Maneno haya yanatofautiana kwa Macarthur J & Mayhue, R (Ed) A Systematic Summary of Biblical Truth: Biblical Doctrine. 591 36 Herman Bavinck, Reformed Dogmatics (p. 523). Baker Publishing Group. Kindle Edition. 35

76

namna fulani ingawa yanakaribiana sana. Wakristo wamezoea wazo kwamba "wokovu" huja kwa imani, haswa pale wanapopinga wokovu

kwa

matendo.

Ingawa

imani

inatumika kwa kila nyanja ya maisha ya Kikristo, ina umuhimu maalum linapokuja suala la kuhesabiwa haki kwa wateule wa Mungu. Kuhesabiwa haki ni tendo la Mungu ambapo

anaweka

haki

ya

Kristo

kwa

mteule, na anatangaza kwamba mteule huyu ni mwadilifu kwa msingi wa haki ya Kristo.

Katika

WCF/11/1

tunasoma

kwamba, “wale ambao Mungu amewaita, pia amewahesabia haki. Yeye hajaweka haki ndani yao lakini anasamehe dhambi zao na kuwakubali kana kwamba ni waadilifu, sio kwa sababu ya kitu chochote kinachofanya kazi ndani yao au kinachofanywa na wao, 77

lakini kwa ajili ya Kristo peke yake. Mungu hazingatii imani yao; yaani kile kitendo cha kuamini, kama ndiyo haki yao au mwitikio wowote mwingine wa utii kwa Injili kwa upande wao. Badala yake, ameweka utii wa Kristo kwao ambapo wao wanapokea na kupumzika juu ya Kristo na haki yake kwa imani (na imani hii sio yao wenyewe lakini ni

zawadi

ya

Mungu.)”

Kifungu

hiki

kinafafanua vizuri asili ya kuhesabiwa haki. Anaposema “yeye haweki haki ndani yao” maana yake ni kwamba Haki ya Kristo inahesabiwa kwao, si kwamba inawekwa ndani yao. Tunapata

ufafanuzi

katika

WLC/70

kwamba, Kuhesabiwa haki ni tendo la neema ya bure ya Mungu kwa wenye dhambi,(Rum. 3:22, 24-25; 4:5) ambapo katika hiyo husamehe dhambi zao zote, 78

huwapokea na kuwahesabia haki machoni pake; (II Kor. 5:19, 21; Rum 3: 22-25, 2728) siyo kwa kitu walichofanya kwa ajili ya kupokea haki hiyo(Tit. 3: 5, 7; Efe. 1: 7) bali ni kwa utii na utoshelevu kamili wa Kristo (Rum.

4:

6-8;

5:

17-19

na

wao

hupokelewa kwa imani tu.(Mdo 10:43; Gal. 2:16; Fil. 3: 9). Ni

tendo

la

Kimahakama

zaidi;

kwamba Kristo alisimama kama mtetezi wetu, kama wakili wetu. Tulisitahili mauti, lakini

Kristo

alilipa

deni

hilo

pale

Msalabani. Watu wengi hujiuliza, kwani Mungu alishindwa kumwokoa mwanadamu kwa njia nyingine mpaka kuruhusu Yesu afe Msalabani? Jibu litakuwa jepesi kwa upande wa Mungu, kwamba inawezekana Mungu angeweza kutumia njia nyingine, lakini muhimu hapa ni kwamba Mungu 79

katika umilele wake tayari aliandaa wokovu wa wateule kupitia mwanaye Mpendwa Yesu Kristo. Mungu anahukumu dhambi, kile ambacho Kristo alikifanya pale msalabani ilikuwa ni kurithisha haki ya Mungu. Kwa hiyo, WCL/71 ipo sahihi kusema kwamba…kwa sababu Mungu, anakubali kuridhika kwa malipo ambayo yalitolewa na Kristo

yaliyopaswa

waliohesabiwa

haki,

kulipwa Yeye

na

mwenyewe

alijitolea malipo haya kupitia kwa Mwana wake pekee, akaweka haki yake kwao; na hahitaji kitu chochote kutoka kwao ili kuhesabiwa haki isipokuwa imani pekee, ambayo pia ni zawadi kutoka kwake; kwa hivyo kuhesabiwa haki kwao ni kwa neema ya bure. Kuna wazo jipya, lakini si jipya kwa muktadha

wetu,

kwamba 80

tunahesabiwa

haki kwa imani, WCL/71 inasema, Mungu “hahitaji kitu chochote kutoka kwao (kwetu) ili kuhesabiwa haki isipokuwa imani pekee.” Ufafanuzi rahisi ni kwamba tunahesabiwa haki baada ya kuamini kazi ya Kristo pale msalabani, tunapomwamini Yesu Kristo; hata hivyo, sisi hatuna imani kama

hiyo,

na

badala

yake

Mungu

anatupatia imani hiyo, ndiyo maana inaitwa wakati mwingine “imani ya bure.” Imani hii ni tofauti na kile kitendo cha kuamini kwamba leo kutatokea muujiza, ni tofauti na kuomba kwa imani; ni kujenga tumaini ndani ya moyo wako baada ya kuona kwamba huna msaada mwingine wowote zaidi ya Kristo na kuweka tumaini kwake. Imani

ya

kuhesbiwa

haki

wakati

mwingine huitwa “imani iokoayo.” Jambo la muhimu

hapa

ni

kwamba 81

imani

hiyo

inatoka kwa Mungu. Jambo la muhimu siyo kuamini tu, chanzo cha imani hiyo ni nini? Kwa mfano katika Yakobo 2:19 inasema kwamba, “wewe waamini ya kuwa Mungu ni mmoja;

watenda

vema.

Mashetani

nao

waamini na kutetemeka.” Hapa imani si ile ya

kuhesabiwa

haki.

Mapepo

hayawezi

kuhesabiwa haki. WCL/72

ina

maelezo

ya

kujitosheleza

kwamba, “imani ya kuhesabiwa haki ni neema

iokoayo

ambayo

inafanya

kazi

mioyoni mwa wenye dhambi kwa njia ya Roho Mtakatifu, na Neno la Mungu. Kwa hiyo wenye dhambi wanahakikishwa juu ya dhambi zao na hali mbaya na hugundua kuwa wao au mtu yeyote au kitu kingine chochote hakiwezi kuwaondoa katika hali hiyo ya upotevu na kwa hiyo wanatoa uthibitisho kamili kwa ukweli wa ahadi ya 82

Injili; na wanapokea pumziko juu ya Kristo na haki yake kwa kusamehewa dhambi kama

Injili

inavyotuambia,

na

kwa

kukubalika na kuhesabiwa kuwa wenye haki mbele ya Mungu kwa ajili ya wokovu.” Kwa

hiyo

kazi

ya

imani

katika

kumhesabia mtu haki ni “kumstahilisha mwenye dhambi machoni pa Mungu (Gal. 3:11; Rum 3:28) sio kwa sababu ya neema zingine ambazo huongozana na imani kila wakati, au kwa sababu ya kazi nzuri ambazo ni matunda yake, au kana kwamba neema

ya

linalojitokeza

imani, kutoka

au

tendo

kwake,

lolote kwamba

Mungu aliamuru kwa ajili kuhesabiwa haki kwake,

bali

imani

inakuwa

chombo

ambacho hupokea na kutumia Kristo na haki yake.”

83

Je imani ya kuhesabiwa haki inakuwepo kwa muda gani katika maisha ya Mkristo? Je

inakuwa

katika

hali

hiyohiyo

au

hubadilika? Inakuwaje pale mtu anapoanza kuwa na mashaka na wokovu wake, je imani hii inafanyaje kazi kwake? Maswali hayo yanaweza kupata majibu kutoka kwenye WCF/14/1-3 Zawadi ya imani inafanya uwezekano wa

mioyo

ya

Wateule

kuokolewa

kwa

kumwamini Yesu Kristo. Zawadi hii ni kazi ya Roho wa Kristo ndani ya mioyo ya Wateule (Ebr 10:39, 2Kor 4:13, Efe 1:17-20, 2:8, 1Kor 12:3, Ebr 12:2) na inakamilishwa kwa kawaida na huduma ya Neno.( Rum 10:14,17, Mt 28:19-20, 1Kor 1:21) Pia inaongezwa na kuimarishwa kwa Neno, kwa maombi, na kwa utekelezaji wa sakramenti. (1Pet 2:2, Mdo 20:32, Rum 4:11, Lk 17:5, 84

Rum 1:16-17, Mt 28:19, 1Kor 11:23-29, 2Kor 12:8-10, Lk 22:19, Yn 6:54-56, Lk 22:32) Kwa imani hii, Mkristo anaamini kile kinachofunuliwa

katika

Neno

kuwa

ni

ukweli kutoka kwa Mungu mwenyewe.( Yn 4:42, 1Thes 2:13, 1Yn 5:10, Mdo 24:14).) Kwa

imani

hii,

muumini

pia

hutenda

kulingana na Neno la Mungu. Kwa imani hii, Muumini hujitiisha kwa unyenyekevu na kumtii Mungu na maagizo yake anuwai (Rum 16:26, Mt 22:37-40) Yeye hutetemeka mbele za Mungu (Isa 66:2) na anakubali ahadi zake juu ya maisha haya na maisha ya baadaye.( Ebr 11:13, 1Tim 4:8).)Lakini hatua kuu za imani iokoayo ni kukubali, kupokea, na kupumzika juu ya Kristo (Yn 1:12, Mdo 16:31, Gal 2:20, Mdo 15:11.)

85

Imani hii ina viwango tofauti vya nguvu na udhaifu (Ebr 5:13-14, Rum 4:1920, Mt 6:30, 8:10.) Inaweza kushambuliwa na kudhoofishwa mara kwa mara na kwa njia nyingi, lakini inapata ushindi.( Lk 22:31-32, Efe 6:16, 1Yn 5:4-5, 1Kor 10:13) Waamini huimarika na kuwa na uhakika kabisa kupitia Kristo (Ebr 6:11-12, 10:22, Kol 2:2, 2Tim 1:12) ambaye hukamilisha imani yao (Ebr 12:2.) Ili

kila

kumwamini

mtu

aokolewe

Yesu,

anahitaji

“kumwamini

Yesu

kumetumika katika Injili ya Yohana kama kuhesabiwa

haki.”37

Mifano

ifuatayo

inathihirisha kwamba kuamini, ni lazima. Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha

37

kuhukumiwa;

kwa

Vincent Cheung, Systematic Theology. 199

86

sababu

hakuliamini

jina

la

Mwana

pekee

wa

Mungu.( Yn. 3:18) Basi wakamwambia, Tufanyeje ili tupate kuzitenda kazi za Mungu? Yesu akajibu, akawaambia, Hii ndiyo kazi ya Mungu, mmwamini yeye aliyetumwa na yeye. (Yn 6:28-29) Lakini hizi zimeandikwa ili mpate kuamini ya kwamba Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu; na kwa kuamini mwe na uzima kwa jina lake. (Yn 20:31)

87

SURA YA TANO TOBA NA UTAKASO a. Toba Toba ni nini? Neno toba lina maana ya "kubadili mawazo ya mtu."38 Katika toba, mtenda dhambi huziona dhambi zake kama vile ambavyo Mungu anavyoziona; kama

https://www.gotquestions.org/Kiswahili/toba-nawokovu.html 38

88

mchafu na mwenye kuchukiza, na kuiona hatari kubwa iliyo mbele yake, kwa sababu dhambi zake zinapingana kabisa na asili takatifu na sheria ya haki ya Mungu (WCF/15/2). Wengine huona toba kama “kugeuka” au kuongoka”39 WLC/76 inasema “toba iletayo uzima ni neema iokoayo, ambayo inafanywa na Roho Mtakatifu na Neno la Mungu moyoni mwa mwenye dhambi ambapo mwenye dhambi anahuzunika sana, na anachukia dhambi zake, na kwa hiyo, yeye hubadilika na kumgeukia Mungu, akikusudia na kujaribu kila wakati kutembea naye katika njia zote za utii mpya.” Katika

toba,

utambuzi

wa

mwenye kweli

wa

dhambi dhambi

hufikia yake.

utambuzi wa aina hii hutokea kwa sababu 39

Vincent Cheung, Systematic Theology. 193.

89

Mungu, tayari amekwisha kumzaa mara ya pili na anawezeshwa na Roho Mtakatifu kuzichukia

dhambi

zake

na

kuendelea

kuachana nazo. Tofauti kati ya Kuhesabiwa Haki na Toba ni kwamba katika kuhesabiwa haki, Mungu anaonyesha haki ya Kristo; lakini katika utakaso; Roho wa Mungu husababisha neema, na huwezesha kuitumia. Katika kuhesabiwa haki, dhambi imesamehewa.” Toba haikomei kwenye mhemko tu, bali inahusisha akili, ufahamu na ujuzi wa mtu wa kuweka matumaini yake kwa Mungu. Katika

toba

kuimarika tunaweka

kwa

imani

yetu

Mungu

matumaini

yetu

inaendelea

kwa yote

sababu kwake.

Maarifa au ujuzi ni wa lazima katika toba, kwani haiwezekani kuweka matumaini yetu kwa kitu ambacho hatuna ujuzi wowote 90

nacho. Mungu hutoa ujuzi kama sehemu ya maisha Hutumia

ya

wokovu

mahubiri

wa ya

mwanadamu. neno

lake

ili

kuwavuta watu waje kwake na kutubu dhambi kutoka mioyoni mwao. Huu ni ujuzi wa ajabu ambao ni zao la Roho Mtakatifu. Toba ni ya lazima kwa Wateule kwa sababu hapo ndipo wanapona uchafu wa dhambi zao, hata hivyo si kwa sababu ya toba Mungu anatusamehe dhambi zetu, bali ni kwa sababu ya wingi wa rehema zake; mtu yeyote asijaribu kujisifu. Toba haifanyi sisi tupate wokovu. Hakuna mtu anayeweza kutubu na kuja kwa Mungu, isipokuwa Mungu amvute huyo mtu kwake (Yn 6:44). Matendo

5:31

na

11:18

zinaonyesha

kwamba toba ni kitu ambacho Mungu anatoa - inawezekana tu kwa sababu ya neema

yake.

Hakuna 91

mtu

anayeweza

kutubu,

isipokuwa

Mungu

ampe

toba.

Wokovu wote, ikiwa ni pamoja na toba na imani, ni matokeo ya Mungu kutuvuta kwake,

kuyafungua

kubadilisha

mioyo

macho yetu.

yetu,

na

Uvumilivu

wa

Mungu hutuongoza sisi kutubu (2 Pet. 3:9), kama

ilivyo

wema

wake

(Rum.

2:4).40

Pamoja na ukweli huo, vilevile ni sahihi kwamba bila kutubu kibinafsi tunaweza kukosa matarajio yoyote ya kusahemehewa dhambi zetu, na ufahamu wetu wa kawaida unaweza

kusaliti

WCF/15/3

imani

tunasoma,

yetu. “Ingawa

Katika toba

hairidhishi chochote kwa dhambi na wala haisababishi

msamaha

wa

dhambi(kwa

kuwa msamaha ni tendo la neema ya Mungu katika Kristo) lakini ni muhimu kwa wenye dhambi, na hakuna mtu anayeweza https://www.gotquestions.org/Kiswahili/toba-nawokovu.html 40

92

kutarajia kusamehewa bila toba (Eze 36:3132, 16:61-63, Tit 3:5, Mdo 5:31, Hos 14:2,4, Rum 3:24, Efe 1:7,Lk 13:3,5, Mdo 17:30-31) Katika toba, Muumini hutumia ujuzi wake wa kawaida kutambua dhambi zake; kubwa na ndogo, na hili ni tukio la kukumbuka katika maisha yake, lakini pia ni tukio endelevu ambapo mmoja mmoja hutuba kwa

ajili

ya

dhambi

zake.

Na

hivyo

“Waamini hawapaswi kutosheka na toba ya jumla, badala yake, ni jukumu la kila mtu kujaribu kutubu kila dhambi yake kibinafsi mbele za Mungu (Zab 19:13, Lk 19:8, 1 Tim 1:13,15, Dan 9, Neh 9).” (WCF/15/5) Katika

Biblia,

toba

matokeo

yake

ni

mabadiliko ya tabia. Hiyo ndio sababu ni kwa nini Yohana Mbatizaji aliwaita watu "kuzaa matunda yapasayo toba" (Mat. 3:8). Mtu ambaye kwa kweli ametubu atatoa 93

ushahidi wa maisha yaliyobadilishwa (2 Kor. 5:17.) Toba ya kibiblia ni kubadilisha mawazo

yako

kumgeukia wokovu

kuhusu

Mungu

(Mdo

Yesu

katika

3:19).

Kristo imani

Kugeuka

na kwa

kutoka

dhambi sio fafanuzi sahihi ya toba, lakini

ni

mojawapo

ya

matokeo

ya

kweli, toba iliyoweka misingi yake katika kuelekea kwa Bwana Yesu Kristo. Je maneno haya ni sawa? Kuungama, Kutubu na Kuomba Rehema? Mara nyingi wanazuoni hujaribu kutofautisha maneno haya na kuyafafanua kila moja kwa maelezo yake. Ingefaa tuone ufafanuzi mmojawapo. Kuungama ni sawa na kukiri au kukubali. Kwa

kiingereza

wanasema

“confess.”

Kuungama ni kukiri na kukubali kwa kinywa chako makosa yako uliyofanya. Wengine

husema

kwamba 94

kuungama

dhambi maana yake ni kujuta kwa ajili ya dhambi

ambazo

mtu

ametenda,

huku

wakitofautisha na dhana ya kutubu kwa kudai kwamba kutubu ni pale ambapo mtu ametambua hali yake ya asili. Wanadai kwamba mtu baada ya kuokoka hahitaji tena kutubu bali anapaswa kuungama tu. Maandiko haya yanashadidia hoja hii: 1 YOH. 1:9-10 Tukiziungama dhambi zetu, Yeye

ni

mwaminifu

na

wa

haki

hata

atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu hatukutenda kuwa mwetu.

wote.

Tukisema

dhambi,

mwongo Fungu

wala hili

kwamba

twamfanya neno

lake

Yeye halimo

linazungumzia

mtu

ambaye tayari ni Mkristo, lakini kwa sababu ya asili ya dhambi kuna uwezekano wa kutenda dhambi katika maisha haya, na hivyo anapaswa kuungama dhambi zake 95

kila mara. Pia tunasoma katika Mithali 28: 13 Afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali yeye

aziungamae

na

kuziacha

atapata

rehema.” Katika neno “kutubu” mara kwa mara linatumika

kwa

waongofu

wapya.

Kwa

mfano katika Matendo ya Mitume 3:19, “Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe,

zipate

kuja

nyakati

za

kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana.” Hapa

dhambi

inayozungumziwa

ni

ile

dhambi ya asili. Maneno

kuomba

rehema

yawezekana

yakawa ni misamiati yenye kurejelea kitu kilekile cha kutubu na kuungama dhambi. Hata hivyo, katika kuomba rehema inaweza kujumuisha matukio fulani fulani kwa nia ya kuhurumiwa na Mungu. Mara nyingi hutokea hasa pale ambapo matokeo ya 96

dhambi

yamejidhihirisha

katika

maisha

yetu. b. Utakaso WLC/75 inasema “Utakaso ni kazi ya neema ya Mungu, ambapo Wateule wa Mungu, waliochaguliwa kuwa watakatifu kabla ya msingi wa ulimwengu, kwa wakati, kupitia kazi ya Roho Mtakatifu hutumia (apply) kifo na

ufufuko

wa

Kristo

kwa

ajili

yao,

huwafanya upya katika miili yao wote kwa mfano wa Mungu. Hupewa mbegu za toba iletayo

uzima,

na

neema

ziokoazo

zinaongezeka na kuwa na nguvu, kwamba wanazidi kufa kwa dhambi, na kuwa hai katika maisha mapya. Tunasoma

katika

WCF/13/1

kwamba,

“wale ambao wameitwa na kuzaliwa upya wana moyo mpya na roho mpya iliyoundwa ndani yao. Kwa kweli wametakaswa kwa 97

nguvu ya kifo cha Kristo na ufufuo na kwa Neno lake na Roho anayeishi ndani yao. Nguvu ya dhambi inayotawala juu ya mwili wote imeharibiwa, na tamaa za ubinafsi za kidunia

zinazoofishwa.

Wakati

huohuo

uwezo wa kutenda utakatifu wa kweli, ambapo bila huo hakuna atakayemwona Bwana

unaimarishwa

na

neema

zote

ziokoazo.” Wanateolojia hutumia neno Kutakaswa kwa maana mbili; Kwanza utakaso kama tukio la mara moja kwa

Mkristo

kutoka

ambapo

kwenye

kwamba

yeye

dhambi

hatawaliwi

anapumzika

yake

tena

na

ya

asili;

dhambi.

Kwamba hatendi dhambi tena kwa sababu tayari

amekwisha

kutakaswa.

Kwamba

Mungu amemtakasa Mkristo na kumtenga na ulimwengu. Maandiko ya kuthibitisha 98

wazo hili ni pamoja na Yohana 15:3 “Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililowaambia.” Pili, utakaso kama tukio endelevu, ambapo inahusisha

Mkristo

katika

ukuaji

wa

polepole katika maarifa na utakatifu, ili kwamba baada ya kupokea kuhesabiwa haki,

sasa

anaweza

kukuza

haki

ya

kibinafsi katika fikira na mwenendo wake. Watu wengine hufanya makosa kufikiria kwamba utakaso ni kama kuhesabiwa haki kwa maana ya kwamba ni tendo la Mungu mara la moja ambapo yeye hutufanya watakatifu

kamili

katika

fikira

na

mwenendo, na hii inamaanisha kwamba Wakristo

wa

kweli

dhambi.

99

hawawezi

kufanya

Hata hivyo, ingawa utakaso huanza wakati wa kuzaliwa upya, Biblia inaelezea kuwa ni mchakato wa ukuaji, ili mtu azidi kufikiria na

kutenda

Mungu,

na

kwa hivyo

njia

inayompendeza

aendelea

kila

siku

kufanana na mfano wa Kristo. Na kwa sababu

hiyo,

inakuwa

vigumu

katika

maisha haya kutakaswa kikamilifu kwa sababu

tunaishi

katika

ulimwengu

uliopotoka. WCF/13/2 inasema “…lakini hawawezi kuwa wakamilifu katika maisha haya. Asili ya zamani ya dhambi inajaribu kuthibiti mwili, akili, na roho. Na hivyo vita vya daima na visivyopatana vinaendelea kwa kila Mwamini. Asili ya zamani inajaribu kupingana na Roho, na Roho anapigana kudai mamlaka yake juu ya mwili.” Katika kushiriki

utakaso,

Wakristo

kikamilifu. 100

Katika

wanapaswa matukio

mengine

ya

wokovu,

ushiriki

wa

mwanadamu ni mdogo sana, na pengine tunaweza kusema hamna ushiriki, bali ni kazi ya Mungu asilimia mia; lakini katika utakaso, mwanadamu anapaswa kushiriki. Kuacha

kuishi

kuungama

maisha

ya

siku

ili

kila

dhambi,

na

kutakaswa.

Anapaswa kuelekeza moyo na mawazo yake katika kumtii Mungu kikamilifu. anasema sehemu

“Mkristo yake

anapaswa

katika

utakaso,

Vincent

kuchukua na

kwa

makusudi afanye maisha ya utii kwa Mungu "kwa hofu na kutetemeka."41 Tunasoma katika Wafilipi 2:12-13 Basi, wapendwa wangu, kama vile mlivyotii sikuzote, si wakati mimi nilipokuwapo tu, bali sasa zaidi sana

mimi

nisipokuwapo,

utimizeni

wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na

41

Vincent Cheung, Systematic Theology. 206

101

kutetemeka. Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.” Kwa maelezo mengine, hata katika juhudi zetu za kumtii Mungu, ni dhahiri kwamba Mungu ndiye hutenda kazi ndani yetu, na si kwa nguvu zetu wenyewe. Utakaso hauwezi kukamilika katika maisha haya kwa sababu ya mabaki ya dhambi iliyo ndani ya kila sehemu yao, na tamaa za “mwili dhidi ya roho;” (WLC/78 na kwa hiyo ni lazima kila siku kutakaswa na Roho Mtakatifu na kuendelea kudumu katika imani yetu kwa Kristo. Kama asemavyo Bakize kwamba “shughuli za ukombozi wa mwanadamu zilikusudiwa ziwe

endelevu”42

na

mojawapo

ya

Leonard Herman Bakize, Ili Niokoke ninahitaji Kanisa (Dar es salaam: EWCP,2019) 29 42

102

mwendelezo

huo

kwa

upande

wangu

ninadhani ni utakaso. Haukamiliki katika Maisha haya. Unaendelea mpaka mwisho wa Maisha yetu hapa duniani. Maswali fikirishi 1. Je,

kwa

kuwa

Wakristo

wametakaswa, je ni wakamilifu? 2. Je, ni watu wanaposema “usijihesabie haki” wana maanisha nini haswa?

SURA YA SITA KUFANYWA WANA Kufanywa wana ni kitendo cha Mungu ambapo huwaingiza wateule katika familia 103

yake, kwa hiyo wanaitwa watoto wa Mungu. katika Yohana 1:12 tunasoma, “Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.” Labda

pengine

tujiulize

maswali

kadhaa, je wale ambao si wateule hao si watoto wa Mungu? Kuna dhana kwamba watu wote ni watoto wa Mungu. Nasita kukubaliana na dhana hii, ingawa pengine naweza

kukubali

kwamba

watu

wote

waliumbwa na Mungu, lakini linapokuja suala la kuwa wana linapaswa kuchukuliwa kwa upekee sana. Biblia inazungumzia habari ya watu wengine kuwa “wana wa Ibilisi” (Shetani). Maandiko yafuatayo yanathibitisha hoja hii;

104

Mathayo 13:38 “lile konde ni ulimwengu; zile mbegu njema ni wana wa ufalme; na yale magugu ni wana wa yule mwovu.” Yohana 6:70 “Yesu akawajibu, Je! Mimi sikuwachagua ninyi Thenashara, na mmoja wenu ni shetani?” Yohana 8:44 “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi,

na

tamaa

za

baba

yenu

ndizo

mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo.” Matendo 3:10 “akasema, Ewe mwenye kujaa hila na uovu wote, mwana wa Ibilisi, adui wa haki yote, huachi kuzipotoa njia za Bwana zilizonyoka?” 105

1 Yohana 3:10, 12 “Katika hili watoto wa Mungu ni dhahiri, na watoto wa Ibilisi nao. Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.”…“si kama Kaini alivyokuwa wa yule mwovu,

akamwua

ndugu

yake.

Naye

alimwua kwa sababu gani? Kwa sababu matendo yake yalikuwa mabaya, na ya ndugu yake yalikuwa ya haki.” Kwa sababu hiyo, ni vigumu kukubali kwamba wasio Wakristo nao ni watoto wa Mungu. Mara nyingi napenda kutumia neno “watu wa Mungu” na wala si “watoto wa Mungu.” Neno “mtoto” au “mwana” lina upekee sana. Mwana ana hadhi tofauti na mtu au kiumbe cha Mungu kinginecho. Biblia inathibitisha wazi kwamba wale waliomwamini Yesu Kristo, yaani wateule wamefanywa kuwa wana wa Mungu, na 106

hivyo wanakuwa na sifa tofauti na wengine. Neno la Mungu linasema “Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio

wana

wa

Mungu.

Kwa

kuwa

hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba, yaani, Baba. Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye. (Rum. 8:14-17) Hatujui

kwa

hakika

ni

katika

mchakato upi tunafanywa wana, lakini Biblia inathibitisha kwamba kwa kuwa sisi ni Wakristo, basi tu wana, na ndivyo tulivyo. Anasema “Tazameni, ni pendo la 107

namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye.” (1 Yoh. 3:1) Kwa hiyo, mtu anapookoka anakuwa mwanachama wa familia mbili muhimu; kwanza familia ya Mungu, yaani ile familia ya wateule wa Mungu, kwamba anakuwa na ushirika wa karibu na Mungu wake. Pili, familia ya wapendwa katika Bwana, yaani ule ushirika pamoja na waumini wengine. Mtu hawezi kujitenga na familia yake mpya ya Kikristo pale anapokuwa ameokoka. Ingawa bado ana uhusiano wa damu na ndugu zake, bado uhusiano wa kiroho ambao uko kwa Mungu na ndugu zake wa kiroho. Kupitia ushirika wa Wakristo, Biblia inatuambia

kwamba 108

“Kwa

hiyo

kadiri

tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio.” (Gal. 6:10). Katika fungu hili Paulo anaweka mkazo kwa watu kusaidiana, ambapo kwa Wakristo

kipaumbele

cha

kwanza

kinapaswa kuwasaidia Wakristo wengine si vinginevyo. Tuhitimishe mada hii kwa kunukuu WCF/12/1

ambayo

inasema,

“Mungu

anathibitisha kufanywa wana kwa wale wote ambao wamehesabiwa haki kwa ajili ya Mwana wake pekee, Yesu Kristo. Wale waliofanywa wana wanafurahia uhuru na haki za watoto wa Mungu, jina la Mungu limewekwa juu yao, wanapokea Roho wa kufanywa wana, wanaweza kukikaribia kiti cha neema kwa ujasiri, na wamewezeshwa kulia,

Abba,

Baba.

Wamehurumiwa,

wanalindwa, wametengwa, wanarudiwa na 109

Mungu kama baba yao. Hawatupiliwi mbali, Wametiwa

muhuri

mpaka

siku

ya

ukombozi, na kurithi ahadi kama warithi wa wokovu wa milele.

110

SURA YA SABA KUHIFADHIWA, UHAKIKISHO NA KUTUKUZWA a. Kuhifadhiwa Wale ambao wamechaguliwa mapema, wameitwa,

wamezaliwa

wamehesabiwa

haki,

upya

na

kwa

hakika

watavumilia mpaka mwisho. Kwa lugha nyingine wokovu

watu

hao

wao,

kwa

ya

kile

matokeo amekifanya

ndani

hawawezi sababu

wokovu

ambacho yao.

kupoteza ni

Mungu

Ingawa

wao

wanawajibika katika kuamini, hata ile imani haitokani na wao wenyewe. Kwa namna moja au nyingine kusema kwamba mteule anaweza kupoteza wokovu wake ni sawa na kusema kushindwa

kwamba kazi

Mungu yake

anaweza

aliyoianzisha

mwenyewe katika maisha ya wanadamu. 111

Tunaposema mtu hawezi kupoteza wokovu wake hatushadidii hata kidogo Maisha ya dhambi,

kwani

yanaonesha

Maisha

wazi

ya

kwamba

dhambi

mtu

fulani

hajaokolewa au si miongoni mwa wateule wa Mungu. Mteule wa Mungu anapaswa kuishi Maisha ya kumpendeza Mungu. Katika

teolojia

neno

linalojulikana

sana kuhusu kuhifadhiwa ni “uvumilivu wa watakatifu.”

Nimeamua

kutumia

neno

“kuhifadhiwa” kwa sababu linalenga hasa kile

ambacho

Mungu

hukifanya

kwa

wateule wanapokuwa katika maisha ya wokovu.

Tofauti

na

matumizi ya

neno

“uvumilivu wa watakatifu” ambapo mara nyingi Wakristo hudhania kwamba kwa sababu ya uvumilivu wao wanaweza kupata wokovu.

John

Frame

anaona

kwamba

maneno haya mawili hayana tofauti kwa 112

sababu

yanaelekea

kuelezea

kwamba

Mkristo wa kweli hawezi kupoteza wokovu wake.

43

Kuhifadhiwa

humaanisha

kwamba

Mungu ndiye anayeendesha wokovu wa Mkristo, na sio mwamini mwenyewe. Hii haimaanishi

kwamba

Mkristo

anaweza

kuishi maisha yoyote yale yasiyo na wajibu kwa

sababu

Mungu

mwenyewe

ndiye

anayemwendesha. Kwa hiyo siyo wazo la kibiblia kusema kuwa kwa kuwa ni Mungu ambaye hututunza, basi hakuna haja kwetu kufanya kiroho.

bidii Ili

yoyote

tuwajibike

ya

maendeleo

ipasavyo,

ya

Mungu

hutupatia uwezo na ujuzi wa kukua katika maisha yetu ya wokovu.

John M. Frame, Salvation Belongs to the Lord: An Introduction to Systematic Theology (New Jersey: P & R Publishing, 2006), 149 43

113

Kwa

hivyo,

wale

ambao

kweli

wameokolewa, ambao ni wateule wa Mungu, kamwe hawawezi kuanguka katika hali yao ya neema kwa sababu Mungu huwawezesha kuvumilia, lakini pia Mungu huwavumilia mpaka mwisho. Hii inathihirisha kwamba wokovu wa mwanadamu ni tendo la Mungu, na wala si la mwanadamu mwenyewe. Tunasoma katika WCF/17/1 kwamba “wale ambao Mungu amewakubali katika Mwana wake Yesu Kristo, na kwa kweli amewaita na kuwatakasa na Roho wake Mtakatifu, kamwe hawawezi kutoka katika hali yao ya neema. Badala yake, hakika wataendelea katika hali hiyo hadi mwisho na wameokolewa milele.” Uvumilivu

huu

wa

Watakatifu

hautegemei hiari yao lakini kwa amri ya Mungu

ya

uchaguzi 114

isiyobadilika,

inayotokana na upendo wake wa hiari, usiobadilika. Inategemea pia ufanisi wa huduma na maombezi ya Yesu Kristo. Maombezi ya Yesu juu ya ujazo wa Roho Mtakatifu na uwepo wa mbegu ya Mungu inayokaa ndani ya Watakatifu. Inategemea pia

asili

ya

Agano

la

Neema

ambalo

halitanguki. Hizi zote zinathibitisha ukweli wa

kutokubadilika

kwa

uhifadhi

wao.

(WCF/17/2) Walakini,

majaribu

ya

Shetani,

ulimwengu, na tabia zao [Watakatifu] za asili za kimwili, pamoja na kupuuza njia ya kuhifadhiwa kwao, inaweza kusababisha Waamini

kufanya

dhambi

kubwa

na

kuendelea na dhambi hiyo kwa muda. Matokeo yake ni kutokumpendeza Mungu na kumhuzunisha Roho Mtakatifu. Katika hili, baadhi ya matokeo ya neema ya Mungu 115

na faida zake huondolewa kwao, na hivyo wanafanya mioyo yao kuwa migumu, na dhamiri

zao

zinajeruhi,

zinaumiza

na

kuwachukiza wengine, na hivyo kujiletea hukumu ya muda juu yao wenyewe. [Hii haimaanishi kwamba Wateule wanaweza kuondoka katika hali yao ya neema, bali Mungu huwarudi kwa njia mbalimbali, kwa sababu ya maovu yao.] WCF/17/3 Maandiko yanaeleza wazi ukweli wa jambo hili; Wote anipao Baba watakuja kwangu; wala ye yote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe. Kwa kuwa mimi sikushuka kutoka mbinguni ili niyafanye mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenipeleka. Na mapenzi yake aliyenipeleka ni haya, ya kwamba katika wote alionipa nisimpoteze hata

116

mmoja, bali nimfufue siku ya mwisho. (Yn. 6:37-39) Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu. (Fil. 1:6) Nami nawapa uzima wa milele; wala hawatapotea kamwe; wala hakuna mtu atakayewapokonya

katika

mkono

wangu. Baba yangu aliyenipa hao ni mkuu kuliko wote; wala hakuna mtu awezaye kuwapokonya

katika

mkono

wa

Baba

yangu. (Yn. 10:28-29) Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika,

wala

wenye

mamlaka,

wala

yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo, wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, 117

wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu. (Rum. 8:38-39). Kwa sababu hiyo nimepatikana na mateso haya, wala sitahayari; kwa maana namjua yeye niliyemwamini, na kusadiki ya kwamba

aweza

kukilinda

kile

nilichokiweka amana kwake hata siku ile. (2 Tim. 1:12) Bwana ataniokoa na kila neno baya, na kunihifadhi hata nifike ufalme wake wa mbinguni. Utukufu una Yeye milele na milele. Amina. (2 Tim. 4:18) Kwa uchache, mistari hiyo inaonesha namna

ambavyo

mtu

yeyote

ambaye

amemkiri Kristo kwa kweli kutoka moyoni mwake

hawezi

kupoteza

wokovu

kwa

sababu analindwa na Mungu peke yake 118

katika wokovu huo. Fundisho hili halisemi kwamba mtu hawezi kupoteza wokovu ila Mkristo wa kweli hawezi kupoteza wokovu wake. Mkristo wa kweli ni yule ambaye ana "imani ya kweli" (1 Timotheo 1: 5) na inathihirishwa

kupitia

fikra,

mawazo,

mwenendo na usemi wa Mkristo huyo. Fundisho hili halitoi nafasi yoyote ya kutenda dhambi kwa sababu ikiwa mtu atasema kwamba ameokoka, basi ni lazima kuonesha matendo kwa nje. Neno linasema, “mtawatambua kwa matunda yao.” Mtu ambaye

ameokolewa

hadumu

katika

dhambi (1 Yoh. 3: 9). Mtu wa namna hii akitenda dhambi huhuzunika sana moyoni mwake

na

kutubu

haraka.

Ikiwa

mtu

amemkiri Kristo kwa unafiki, mara zote hana maumivu yoyote na dhambi, hutenda dhambi

kwa

kisingizio 119

cha

uhuru

wa

Kikristo. Mtu aliyekiri kinafiki mara nyingi hurudi nyuma na kuanguka haraka wakati wa shida na mateso (Mat. 13:21). Wakati mwingine hata Mkristo wa kweli anaweza kuanguka katika dhambi kubwa, lakini anguko kama hilo kamwe halidumu. Walakini, ikiwa Mkristo kama huyu ataendelea na maisha ya dhambi, hatuna sababu kuamini kukiri kwake kwa imani, na kwa hivyo tunapaswa kumfikiria kama

kafiri.

Na

watu

kama

hawa

wanapaswa kutengwa na kanisa, ikiwa ni pamoja na kufukuzwa kama ikiwezekana ((Mat.18:15-17) Wale ambao wanaanguka kabisa na wanakataa

kutubu

hao

hawajawahi

kuokolewa kwa kweli. Yohana anasema, "Walitoka kwetu.

kwetu,

Maana

lakini

kama 120

hawakuwa

wa

wangalikuwa

wa

kwetu,

wangalikaa

pamoja

nasi.

Lakini

walitoka ili wafunuliwe kwamba si wote walio wa kwetu. (1 Yoh. 2:19). Tunayo mifano kadhaa kwenye Biblia kuhusu watu wanaoonekana kuokoka na baadaye kuanguka moja kwa moja. Kwa mfano Yuda alionekana kumfuata Yesu kwa miaka kadhaa, lakini Yesu anasema, "Je! Mimi sikuwachagua ninyi kumi na mbili? Lakini mmoja wenu ni Ibilisi! "(Yn 6:70). Na mstari waa 64-65 anasema, Lakini kuna wengine miongoni mwenu wasioamini. Kwa maana Yesu alijua tangu mwanzo ni nani wasioamini, naye ni nani atakayemsaliti. Akasema, Kwa sababu hiyo nimewaambia ya kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu

isipokuwa

amejaliwa

na

Baba

yangu. Kwa hiyo mtu anaweza kuonekana katika njia ya unyofu kwa muda, lakini 121

anguko lake linaweza kuthihirisha unafiki wake, ya kwamba hakukiri kutoka moyoni mwake, na kwmaba hakuwa na imani katika Kristo Yesu. Kwa hiyo WLC/61 inasema, “…Sio kila mtu anayesikia Injili na kuwa mshirika katika kanisa linaloonekana ameokoka,

bali

ni

wale

tu

ambao

ni

washirika wa kweli wa kanisa lisiloonekana. (Yn. 12: 38-40; Rum 9: 6; 11: 7; Mt. 7:21; 22:14)” b. Uhakikisho Uhakikisho

si

miongoni

mwa

michakato ya wokovu lakini ni sehemu ndogo

ya

ufafanuzi

wa

“kuhifadhiwa.”

Kwamba mtu anajua ukweli na uhakika wa wokovu wake. Ningependa kufafanua dhana ya uhakikisho wa wokovu kupitia WCF sura ya kumi na nane kwa kuzingatia sehemu zake zote:122

Wanafiki na wasiozaliwa mara ya pili wanaweza uongo

kujidanganya

na

hisia

wanampendeza

za

Mungu

na

tumaini

mwili na

la

kwamba kwamba

wameokolewa. Walakini hisia zao zitakufa pamoja nao. Wale wanaomwamini kwa kweli Bwana Yesu, wanaompenda kwa dhati na wanajaribu kutembea kwa dhamiri njema mbele yake, wanaweza kuwa na hakika katika maisha haya, kwamba wapo katika hali ya neema. Wanaweza pia kufurahi katika tumaini la utukufu wa Mungu, na hawataona

aibu

kwa

tumaini

hilo.

(WCF/18/1) Uhakikisho huu haujaegemea katika tumaini la kubahatisha au kukisiakisia tu. Na badala yake, ni uhakikisho usiotanguka wa imani iliyowekwa juu ya ukweli wa ahadi za

Kimungu

za

wokovu. 123

Pia,

kuna

uthibitisho kiroho,

wa

ndani

ambao

wa

ufahamu

tumepewa

na

wa

Mungu,

ambapo ahadi hizi zinatimilizwa. Na kuna ushuhuda wa Roho wa kufanywa watoto, akishuhudia pamoja na roho zetu kwamba sisi ni watoto wa Mungu. Roho huyu ndiye kiapo cha urithi wetu. Kwa yeye tumetiwa muhuri

mpaka

siku

ya

ukombozi.

(WCF/18/2) Uhakikisho

huu

usiotanguka

sio

muhimu sana kwa imani, kwani Mwamini wa kweli hawezi kuwa na mashaka na migongano juu uhakikisho huu, wakati mwingine

hungoja

kwa

wakati

mpaka

uhakikisho huo utakapokua ndani yake [Hoja hapa ni kwamba kama binadamu, haimaanishi kwamba uhakikisho ni sehemu ya imani. Mtu anaweza kuwa na mashaka na

migongano

ya

kiimani 124

ndani

yake.

Wakati mwingine anaweza kujiona kama hayuko salama, lakini kitu cha muhimu ni kwamba anakua katika uhakikisho huo mpaka kurudi kwa Kristo]. Lakini kwa kuwa Roho huwawezesha Waamini kujua vitu walivyopewa na Mungu kwa bure, kila Mwamini anaweza kujawa na uhakikisho kamili wa wokovu na kazi ya kawaida ya Roho pasi na ufunuo usio wa kawaida. Kwa hiyo ni jukumu la kila Mwamini kujua ukweli wa wito wake na uchaguzi, ili moyo wake ujazwe na amani, furaha katika Roho Mtakatifu, upendo, kumshukuru Mungu, na furaha ya utii, ambayo ndiyo matokeo ya uhakikisho. Uhakikisho hautufanyi tuishi maisha ya dhambi bali kuepuka kuishi maisha ya dhambi ya aina yoyote ile. [Kwa hiyo,

wale

wanaofanya

dhambi

kwa

kisingizio cha uhakikisho wa wokovu wao ni 125

dhahiri

kwamba

bado

wapo

gizani,

wanahitaji mwangaza wa kuona mambo ya kiroho; au labda pengine si Wateule, bali ni waovu walioitikia wito kwa huduma ya Neno,

na

kamwe

hawataokolewa].

(WCF/18/3) Hata Waamini ambao wana uhakika kuwa

wameokolewa

wanaweza

kuyumbishwa [kutikiswa]. Wakati mwingine wanaweza kuwa na uhakika kidogo au kupoteza kwa muda uhakika huu. Hii inaweza

kutokea

kwa

sababu

kadhaa:

kwanza, ikiwa hawajali kuwa wanaweza kuanguka katika dhambi fulani ambazo huumiza dhamiri zao na kumhuzunisha Roho Mtakatifu, pili ikiwa watajaribiwa ghafla, na tatu, ikiwa Mungu ataondoa mwangaza

wa

uwepo

wake

kwao,

na

matokeo yake hata yule anayemwogopa 126

Mungu,

kwa

muda

anaweza

kutembea

gizani. Walakini, kamwe mbegu ya Mungu ndani yao haitoki; yaani maisha ya imani, upendo wa Kristo na upendo wa Waamini wengine, moyo wa dhati na dhamiri ya utii, ambayo kwa hiyo Roho anaweza kufufua tena

uhakikisho

huu

kwa

wakati

ili

wasipotee gizani kabisa (WCF/18/4) c. Kutukuzwa Hatimaye tunafikia tamati ya mpangilio wa wokovu

wa

mwanadamu.

Kwa

kuwa

waumini huvumilia hadi mwisho, baraka yao ya mwisho isiyoepukika ni kutukuzwa. Katika

soteriolojia

ya

Kikristo

wengi

tunaamini kwamba hili ni tukio la baadaye. Ni

tukio

hugawanywa

katika

vipengele

viwili; a) wakati wa kufa b) wakati wa kurudi kwa Bwana wetu Yesu Kristo hapa duniani.

Kwa

upande 127

wangu

naamini

kwamba kipengele cha pili ndicho chenye ufanisi zaidi kuliko kile cha kwanza. Hii inatokana

na

ukweli

kwamba

ingawa

Mkristo anapokufa anakuwa na ushirika na Kristo, hata hivyo ushirika huo haukamiliki mpaka Ufufuo wa wafu. Ufufuo wa wafu ndio

ukamilifu

wa

kutukuzwa

kwa

Wakristo. Katika kutukuzwa, dhambi zinaondolewa kabisa katika maisha ya watakatifu katika hali ya milele (Rum 8:18; 2 Kor.

4:17).

Wakati wa kuja kwa Kristo, utukufu wa Mungu (Rum. 5: 2) -Heshima yake, sifa, ukuu, na utakatifu-vitatambuliwa ndani yetu; badala ya kuwa wanadamu wenye kulemewa

na

tutabadilishwa

asili kuwa

ya

dhambi,

watakamilifu

wasiokufa na tutafurahia ushirika wetu kamili na Kristo milele yote. 128

SURA YA NANE TULIP Ukalviniti kufupisha

kwa

huelezea kutumia

wokovu neno

kwa TULIP

ambayo ni finyazo ya maneno ya Kiingereza. Mara nyingi hujulikana kama hoja tano za 129

Ukavinisti

kuhusu

linawakilisha

hoja

wokovu.

Kila

neno

muhimu;

na

ndiyo

maana wakati mwingine huandikwa pamoja na nukta T.U.L.I.P T-Total depravity (Upotovu Kamili) U-Unconditional

election

(Uchaguzi

usiokuwa na masharti) L-Limited

atonement

(Upatanisho

wenye

Mipaka) I-Irresistible

grace

(Neema

Isiyoweza

Kuzuiliwa) P-Perseverance of the saints. (Uvumilivu wa Watakatifu) T-Total depravity (Upotovu Kamili) Baada Anguko mwanadamu aliingia katika hali ya dhambi. Kwa kweli dhambi imeenea

katika

kila 130

hali:

moyo,

hisia,

mapenzi, akili, na mwili. Hii inamaanisha kwamba

watu

hawawezi

kujitegemea

kumchagua Mungu, kwa sababu sehemu zao zote muhimu za utambuzi zimepotoka kabisa.

Ni

upotofu

kamili,

kwa

hiyo

mwanadamu hawezi kujiokoa mwenyewe. Ni lazima Mungu aingilie kati ili kutatua tatizo hili la dhambi. Ijapokuwa

tunao

ufahamu

wa

kawaida wa uumbaji wa Mungu kupitia vitu vinavyoonekana, bado ufahamu wa namna hii

hauwezi

kumchagua

kutusaidia Mungu.

kumjua

Utashi

huru

na wa

mwanadamu umepotoshwa, na hivyo mara zote huelekea maovu. Hata matendo mema ya mwanadamu hayasaidii kitu chochote kwa

sababu

nayo

yamepotoka.

anahitajika kuingilia kati tatizo hili.

131

Mungu

Kwa hiyo, ni lazima Mungu afanye kazi yote ya wokovu, kuanzia kuwachagua wale ambao wataokolewa na kuwatakasa katika maisha yao yote hadi watakapokufa na kwenda mbinguni. (Mk. 7: 21-23, Rum. 6:20, 1 Kor. 2:14). U-Unconditional election (Uchaguzi usiokuwa na masharti) Mungu

anachagua

ni

nani

atakayeokolewa bila masharti na vigezo vyovyote.

Kwa

sababu

watu

wamekufa

katika dhambi zao, hawawezi kuwa na mwitikio kwa Mungu. Katika umilele wake Mungu aliwachagua watu fulani kuokolewa. Watu waliookoka wanaitwa Wateule. Mungu huwachagua sio kwa tabia zao kibinafsi au sifa,

lakini

kwa

sababu

ya

fadhili

na

mapenzi yake. Kuchaguliwa katika wokovu hautokani na ujuaji wa Mungu wa nani 132

atakayekuwa na imani katika siku zijazo. (soma ufafanuzi wa kutosha kwenye mada ya kutangulia kuchaguliwa) L-Limited atonement (Upatanisho wenye Mipaka) Upatanisho wenye mipaka ni hoja kwamba Yesu Kristo alikufa tu kwa ajili ya dhambi za wateule. Mara nyingi fundisho hili hupotoshwa kwa kutokujua “ukamilifu wa

dhabihu

ya

Kristo.”

Kristo

alijitoa

dhabihu pale msalabani, na kwa hiyo kwa vyovyote vile dhabihu yake ni kamilifu na inawafanya

kamili

wale

ambao

kwao

imefanyika. Haiwezekani dhabihu ya Kristo ikashindwa kutimiza makusudi yake. Ikiwa tutasema kwamba dhabihu ya Kristo ni kwa watu wote, basi tunahitaji pia kuamini

kwamba

watu 133

wote

duniani

wataokolewa,

na

hapo

tutakuwa

tumetumbukia kwenye dhana ya “wokovu kwa wote” (universal salvation). Kwa hiyo tunasema kwamba Yeyote ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake, ni lazima ataokolewa. Na pia ni sahihi kusema kwamba watu wote hawataokolewa;

kuna

wengine

ambao

wataenda motoni, na wengine mbinguni. I-Irresistible grace (Neema Isiyoweza Kuzuiliwa) Neema inamaanisha

isiyoweza kwamba

isiyozuiliwa

Mungu

huwaleta

Wateule wake kwenye wokovu kupitia wito wa

ndani,

ambao

hawana

nguvu

ya

kuipinga. Roho Mtakatifu huwapatia neema mpaka watubu na kuzaliwa mara ya pili. (ufafanuzi kuhusu hoja hii uko katika mada ya kuitwa)

134

P-Perseverance of the saints (Uvumilivu wa Watakatifu) Hoja kwamba

hii

imejikita

wateule

katika

hawawezi

ukweli kupoteza

wokovu wao. Kwa sababu wokovu ni kazi ya Mungu Baba; Yesu Kristo, Mwokozi; na Roho Mtakatifu, kwa hiyo haiwezi kuzuiliwa. Hakuna

ambaye

atapotea,

yuko

Mungu

salama

amemwita

mikoni

mwake

milele. Hata hivyo, wateule hawana nguvu ya kuvumilia mpaka mwisho, ila Mungu ndiye anayevumilia,

sio

watakatifu

wenyewe.

Mafundisho ya Ukalvini juu ya uvumilivu wa watakatifu ni tofauti na teolojia ya Kilutheri

na

wanashikilia

Kanisa kwamba

kupoteza wokovu wao.

135

Katoliki watu

ambao

wanaweza

Vifupisho vya TULIP hupanga hoja tano

za

Ukalvini

kimwendelezo, nyingine.

Kwa

na

kimantiki

kila

mfano

na

hoja

inategemea

ikiwa

wanadamu

wamepotoka kabisa, basi wao hawawezi kuanza

kumwitia

Mungu,

hawawezi

kumchagua Mungu. Mungu lazima awaite watu kwenye wokovu kupitia uchaguzi usio na masharti. Mungu lazima pia atoe njia ya wokovu kwa kifo cha Yesu Kristo. Mungu hufanya wokovu udhihirike kwa wito wenye ufanisi wa Roho Mtakatifu. Anawaweka salama wale waliookolewa ili warithi uzima wa milele ambao amewaahidi.

Hitimisho

136

Wokovu ni zawadi ya Mungu kwa manadamu aliyepotoka. Mwanadamu huyu huipokea zawadi hii kwa imani katika Yesu Kristo na kujitoa ili kusamehewa dhambi. Tunaamini

kwamba

mwanadamu

huhesabiwa haki kwa neema kwa imani na si kwa matendo (Mdo. 13:38-39, Rum. 6:23, Efe. 2:8-10). Tunaamini kwamba wateule wote

wameokolewa

na

wataokolewa

na

kuhifadhiwa salama milele (Rum. 8:1, 3839; Yn. 10:27-30)

137

Marejeleo Bakize,

Leonard

Herman.

Ili

Niokoke

ninahitaji Kanisa (Dar es salaam: EWCP,2019) 29 Bavinck,

Herman.

Reformed

Dogmatics.

Baker Publishing Group. Kindle Edition.

138

Brown,

John.

Systematic

Theology:

A

compendious View of Natural and Revealed Religion (Grand Rapids: Reformation

Heritage

Books,

2002) Bruce Demarest, The Cross and Salvation (Wheaton: Crossway Books, 1997) Charles Ryrie, Basic Theology: A Popular Systematic Guide to Understanding Biblical Truth. Kindle Edition Cheung,

Vincent.

Systematic

Theology

(Michigan: Zondervan Publishing House, 2003) Erickson J. Millard, Christian Theology (3rd Ed)

(Grand

Academic, 2013)

139

Rapids:

Baker

Geoffrey. W Bromiley, Historical Theological: An

Introduction

(T&T

Clark:

Edinburgh,1979) Grudem,

Wayne.

Systematic

Theology

(Grand Rapids: MI: Inter-Varsity Press 1994),678. Hodge, Charles, Systematic Theology – (Vol. III) (Grand Rapids, MI: Christian Classics Ethereal Library,) John M. Frame, Salvation Belongs to the Lord: An Introduction to Systematic Theology (New Jersey: P & R Publishing, 2006) Kunhiyop, Samuel Waje. African Christian Theology

(Kenya:

2012)

140

HippoBooks,

Louis Berkhof, Systematic Theology (Grand Rapids: Eerdmans, 1974) Macarthur J & Mayhue, R (Ed) A Systematic Summary of Biblical Truth: Biblical Doctrine

(Wheaton,

Illinois:

Crossway, 2017) Martin Luther, The Bondage of the Will; (Grand Rapids, Michigan: Fleming H. Revell, 2000) Reymond, L. Robert, A New Systematic Theology of The Christian Faith (Nashville:

Thomas

Nelson

Publishers 1998) Sinclair B. Ferguson, The Christian Life: A Doctrinal

Introduction

Pennsylvania:

The

Truth Trust, 1997) 141

(Carlisle,

Banner

of

142